Monday, April 18, 2016

MAGUFULI AMTEUA CHIKAWE KUWA BALOZI WA TANZANIA NCHINI JAPAN

MAJALIWA AMPA POLE MBOWE KWA KUFIWA NA KAKA YAKE

MAJALIWA AMPA POLE MBOWE KWA KUFIWA NA KAKA YAKE
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na  Mwenyekiti wa CHADEMA na kiongozi wa Upinzani Bunge, Freeman Mbowe  wakati alipokwenda kumpa pole  kufuatia kifo cha kaka yake, Kanali Mstaafu Maximillian Aikaeli Mbowe, nyumbani kwa marehemu, Tegeta jijini Dar es salaam Aprili 16, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akitia saini kitabu cha maombolezo ya kifo cha kaka yake   Mwenyekiti wa CHADEMA na kiongozi wa Upinzani Bunge, Freeman Mbowe   (kulia kwake) wakati alipokwenda kumpa pole  kufuatia kifo cha kaka yake, Kanali Mstaafu Maximillian Aikaeli Mbowe, nyumbani kwa marehemu, Tegeta jijini Dar es salaam Aprili 16, 2016.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana akisalimiana na wanafamilia wakati alipokwenda  kumpa pole   Mwenyekiti wa CHADEMA na kiongozi wa Upinzani Bunge, Freeman Mbowe     kufuatia kifo cha kaka yake, Kanali Mstaafu Maximillian Aikaeli Mbowe, nyumbani kwa marehemu, Tegeta jijini Dar es salaam Aprili 16, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na mwanasiasa mkongwe,Kingunge Ngombale- Mwiru  wakati alipokwenda  kumpa pole   Mwenyekiti wa CHADEMA na kiongozi wa Upinzani Bunge, Freeman Mbowe     kufuatia kifo cha kaka yake, Kanali Mstaafu Maximillian Aikaeli Mbowe, nyumbani kwa marehemu, Tegeta jijini Dar es salaam Aprili 16, 2016.

Ratiba ya Mkutano wa Bunge la Bajeti 2016/17 Linaloanza Kesho Tarehe 19 Hadi Mwezi wa 7 Tarehe 1

Ratiba ya Mkutano wa Bunge la Bajeti 2016/17 Linaloanza Kesho Tarehe 19 Hadi Mwezi wa 7 Tarehe 1

Mkutano wa Tatu (3) wa Bunge la Kumi na Moja (11) unatarajia kuanza mjini Dodoma kesho tarehe 19 Aprili 2016. Mkutano huu ni mahususi kwa ajili ya kujadili na kupitisha Bajeti ya Serikali.

Wabunge wote wametakiwa kuwasili mjini Dodoma siku ya Jumapili tarehe 17 Aprili 2016

Picha mbali mbali za CDTI juzi.

Hali tete kwa rais wa Brazil

Hali tete kwa rais wa Brazil

  • Saa 2 zilizopita
Image copyright AP
Image caption Brazil: Chuma cha rais Dilma Rousseff ki motoni
Upinzani nchini Brazil umefanikiwa kupata theluthi mbili ya kura zilizokuwa zikitakiwa katika hatua za kuelekea kupiga kura ya kutokuwa na imani na
Rais wa nchi hiyo Dilma Rousseff.
Maandamano makubwa yanapangwa kufanywa sehemu mbalimbali Brazil, ambako wabunge wanatarajiwa kupiga kura leo, ikiwa wanataka Rais Dilma Rousseff ashtakiwe au la, kwa sababu ya kubadilisha bajeti. Wanaompinga lazima wapate theluthi mbili ya kura zote , kuweza kumshtaki rasmi kiongozi huyo katika baraza la Seneti.
Image copyright AFP
Image caption Wanaompinga lazima wapate thuluthi mbili ya kura zote , kuweza kumshtaki rasmi kiongozi huyo katika baraza la Seneti.
Mamia ya askari polisi wenye silaha wameshika zamu, kujaribu kuzuia makabiliano baina ya waandamanaji wanaopingana, na ambao wamekesha nje katika mji mkuu, Brasilia.
Waandishi wa habari wanasema, kizuizi cha urefu wa mita mbili, kilichowekwa baina ya waandamanaji hao, mahasimu ni ishara ya mgawanyiko mkubwa nchini, baina ya wafuasi na wapinzani wa Rais Rousseff.
Image copyright AFP
Image caption Bi Rouissef anakanusha kuwa alibadilisha hesabu za bajeti
Bi Rouissef anakanusha kuwa alibadilisha hesabu za bajeti, kabla ya uchaguzi wa mwaka 2014, ambapo alichaguliwa tena.
Anawashutumu wanasiasa wanaotaka kuitoa madarakani serikali yake iliyochaguliwa na wananchi wa nchi hiyo.

Saturday, April 16, 2016

VYETI ,VYETI, VYETI ....

VYETI ,VYETI, VYETI .....Vyeti vimeokotwa  , vyeti vya  FADHILI  MASAWE  MICHAEL  kidato cha nne  amemalizia shule ya secondary  GG .SHULUA .iliyoko box 60138.Dar es salam,
Kidato cha sita amesomea  shule ya MWENGE  sec, School baada ya hapo kajiunga na masfunzoo ya JKT kwa muujibu, kikosi cha  BULOMBOLA  .tafahari unaombwa kama unamfaham  au unaweza mfikishia taarifa kuwa vyeti yake vimekotwa viko mahali salama  tuwasiliane kwa no;0755-233755        AU.    0784900291 sambaza ujumbe huu kila group   yawezekana taarifa hizi zikamfikia  ahsanteni sana.👏