Monday, May 10, 2021

VIDONDA VYA TUMBO -AINA, CHANZO, DALILI & TIBA.

UTANGULIZI – UJUE UGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali za kuyeyusha chakula unaoitwa mucus. Kemikali ambayo ni acidi inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni, kama ukuta wenye ute ukiharibiwa na kushindwa kufanya kazi basi kemikali (acid) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo. Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa. Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine kama kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua uzito. AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO Kuna aina zipatazo mbili za Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers) Vidonda vya tumbo kubwa (Gastric ulcers) – Hivi ni vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani kwenye tumbo kubwa 2. Vidonda vya utumbo mdogo (Duodenal ulcers) – Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo (hasa juu) duodenal-ulcer CHANZO CHA VIDONDA VYA TUMBO Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo, vyanzo hivyo ni; Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori) Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu kama asprin, (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine) Kuwa na mawazo mengi Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi Kunywa pombe na vinywaji vikali Uvutaji wa sigara Kuto kula mlo kwa mpangilio DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO Dalili za vidonda vya tumbo hujitokeza baada ya kula au kabla ya kula, ila mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia na endelea kukuza tatizo, vidonda vya tumbo vinadalili kama; gastrita Kupata maumivu ya tumbo yanayokuwa kama ya moto (kuunguza) baada na kabla ya kula Kupatwa na kiungulia karibu na chembe ya moyo Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu Kupata haja kubwa ya rangi kahawia au nyeusi yenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito Kushindwa kupumua vizuri JINSI YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO Kunywa maji mengi Punguza mawazo, fanya mazoezi yatakupunguza na mawazo Punguza (balansi) kiwango cha halemu (choresterol) Usivute sigara Punguza au acha kunywa pombe Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 7 hadi 9 TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO Tatizo la Vidonda vya tumbo linatibika kufuatana na mda wa tatizo, mara nyingi wagonjwa wamekuwa wakizalau dalili za vidonda vya tumbo na kudhani kuwa hakuna madhara makubwa. DAWA YA VIDONDA VYA TUMBO Tuna dawa ya kutibu Vidonda vya tumbo ambayo ni ya asili isiyo na kemikali ambayo hufanya mtu kupona na kuimarika kabisa. Dawa hiyo hutibu kwa mda kulingana na mda wa tatizo, tatizo halirudi tena maana huondoa chanzo pamoja na ugonjwa sio kituliza maumivu, ukianza kutumia baada ya wiki moja mgonjwa huanza kupona na huonesha mabadiliko, pia mgonjwa anapewa mfumo wa maisha ambao inatakiwa autumie kwasababu kuna mtindo wa maisha unaendelea kuongeza tatizo pia kuna mtindo unapunguza hatari ya ugonjwa. Tunamshukru Mungu kwa uumbaji wake na kutupa dawa ambazo alizileta ili kutuimarisha na kutuponya, Mungu hakuumba dawa nyingine zaidi ya mimea na vitu vingine vya asili, japo wengi hudharau. Mungu tunaomba utuokoe na kutuponya. MAWASILIANO roryamaendeleo@gmail.com 0768441610

Tuesday, September 12, 2017

RAIS DK. MAGUFULI AMUAPISHA JAJI MKUU FROF. IBRAHIM HAMIS JUMA, 

 Rais Dk John Magufuli akimuapishaJaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma  leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Profesa Ibrahim anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mkuu Mstaafu Othman Chande na kuwa jaji wa nane kushika wadhifa huo tangu nchi ipate uhuru huku akiwa Mtanzania wa sita. Wapili kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi

 Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma akisaini hati ya kiapo mara baada ya kuapishwa



Rais Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini hati ya kiapo cha Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa Ibrahimu Hamisi Juma baada ya kumuapisha 

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya kiapo Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa Ibrahimu Hamisi Juma 

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza baada ya kumuapisha Jaji Mkuu wa Mahakama Tanzania Mhe. Profesa Ibrahimu Hamisi Juma leo 

Jaji Mkuu wa Mahakama Tanzania Profesa Ibrahimu Hamisi Juma akizungumza baada ya kuapishwa leo 

 Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza baada ya Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahimu Hamisi Juma kuapishwa

 Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi (kushoto) akiteta jambo na  Jaji Mkuu mstaafu Othman Chande (kulia) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju wakati wa hafla hiyo ya kuapishwa kwa Jaji Mkuu wa Tanzania 

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya majaji waliohudhuria hafla ya kumuapisha Jaji Mkuu wa Tanzania 

 Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abbasi akifuatilia kwa makini hafla hiyo

 Jaji Kiongozi Ferdinand Wambaliakiteta jambo na  Jaji Mkuu Mstaafu Othman Chande (kulia) wakati wa hafla hiyo

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa hafla hiyo.  

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Jaji Mkuu Mstaafu Othman Chande baada ya kumuapisha Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahimu Hamisi Jum. Kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai

 Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumz na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi wakati wa hafla hiyo

 Rais Dk. John Magufuli akiwa na Jaji Mkuu na Spika wa Bunge wakati wa hafla hiyo


Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma, Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai na Majaji mbalimbali, mwisho mwa hafla hiyo,leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Sunday, July 16, 2017

UMOJA WA VIJANA WA CCM VYUO NA VYUO VIKUU MKOA WA MWANZA WAKAKABIDHIWA VYETI NA NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA

Sunday, July 16, 2017Mgeni Rasmi Katika Mahafali ya wahitumu wa Vyuo vikuu Mkoa wa Mwanza Ndugu Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Rodrick Mpogolo , Akiongozana na Daniel Zenda K.katibu Idara Vyuo na Vyuo Vikuu , Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndgugu Anthony Dialo, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndg Raymond Mwalimu, Waheshimiwa Wabunge wa Ilemela na Nyamagana pamoja na viongozi wa secretariat ya Mkoa, Katibu wa CCM Nyamagana na viongozi mbali mbali wa Chama cha Mapinduzi, Makundi ya Kijamii, Machinga, wapiga debe, Mama Ntilie na wajasiliamali. Mahafali yaliyofanyika Ukumbi Rock City Mall.

Ndugu Mgeni Rasmi  amewasihi sana wahitimu kuwa Wabunifu wa miradi za kuweza kujitegemea haswa katika Kilimo na Ufugaji, Mgeni Rasmi aliwakumbusha wahitimu kuenenda sawa na Imani ya Ccm kama ilivyoainishwa katika katiba ya CCM Ibara ya nne (4) na   aliwataka wahitimu Wajiajiri(Blue colour Job) na kutumia Maarifa waliyonayo katika Jamii na kuondokana na dhana ya kuajiriwa.

Aliendelea kusisitiza Umuhimu wa Database yani taarifa za wahitimu wote zinaumuhimu sana kwa kutumikia chama cha Mapinduzi na Taifa kwa Ujumla.

Mahafali ya kwanza kubwa Mkoani wanafunzi/Makada walio hitimu 256 na washiriki walio hudhuria 612 wanachama.

Mahafali hiyo ilifana kwa kuanza Shughuli ya kijamii kutembelea kituo cha Watoto waliofanyiwa Ukatili(Foundation Karibu Tanzania) kaimu katibu Idara Vyuo na Vyuo Vikuu ndg Daniel Moses Zenda  aliongoza Shughuli hiyo na kujionea namna Ukatili waliofanyiwa watoto hao. Pamoja na kushiriki na kutoka Mchango Ulioandaliwa na Wanafunzi wa Vyuo Vikuu.

Imetolewa na 
Idara Vyuo na Vyuo Vikuu.

RAIS MAGUFULI NA MKEWE JANETH MAGUFULI WASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI KATIKA PAROKIA BIKIRA MARIA CHATO

, July 16, 2017


Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli pamoja na mke wake Mama Janeth Magufuli wakitoa sadaka wakati wa ibada ya jumapili katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo julai 16, 2017.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na Mkewe Janeth Magufuli wakisikiliza mahubiri toka kwa Padri Henry Mulinganisa wakati wa ibada ya jumapili katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo Julai 16 2017.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisisitiza jambo wakati wa ibada ya jumapili katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo Julai 16, 2017.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliyeshika kikapu cha sadaka akipokea sadaka toka kwa Mke wake Bi Janeth Magufuli wakati wa kuchangia ujenzi na upanuzi wa katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo Julai 16, 2017.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliyeshika kikapu cha sadaka akipokea sadaka kutoka kwa waumini wakati wa kuchangia ujenzi na upanuzi wa katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita. 

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa ameshika kikapu chenye michango ya fedha zilizotolewa na waumini wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa hilo, leo Julai 16, 2017

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru mmoja wa waumini wa kanisa hilo ndugu Mwita Chacha mara baada ya kuchangia mifuko mitano ya saruji kwaaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita .

Mama Janeth Magufuli mke wa Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiahidi mchango wake wa ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akishuhudia mmoja wa waumini wa kanisa hilo ndugu Deogratius Ambrosi mwenye ulemavu wa mkono,akitoa mchango wake wa kiasi cha shilingi elfu tano kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru mmoja wa waumini wa kanisa hilo ndugu Deogratius Ambrosi mwenye ulemavu wa mkono,akitoa mchango wake wa kiasi cha shilingi elfu tano kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwashukuru waumini walioshiki kuchangia ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita,ambapo zilikusanywa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni kumi na tatu pamoja na ahadi mbalimbali za vikiwemo vifaa vya ujenzi.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa nje ya kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita, ambalo linaendelea kupanuliwa na kujengwa hapo akielekea kuwasalimia waumini walio kuwa nje ya kanisa na kuwaaga baada ya ibada.

Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiondoka kwenye kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita, mara baada ya ibada.

Katibu wa Rais Ndugu Ngusa Samike (kushoto) akikabidhi mchango wa Mhe Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli jumla ya shilingi milioni kumi kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita,

Waumini wa kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita wakiwa kwenye ibada.

Jengo la kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita linaloendelea kupanuliwa na kujengwa

Waumini wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita wakitoka kwenye ibada ya jumapili

MAGAZETI YA LEO JULAI 17,2017