Monday, May 10, 2021
VIDONDA VYA TUMBO -AINA, CHANZO, DALILI & TIBA.
Tuesday, September 12, 2017
RAIS DK. MAGUFULI AMUAPISHA JAJI MKUU FROF. IBRAHIM HAMIS JUMA,
Rais Dk John Magufuli akimuapishaJaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma leo Ikulu Jijini Dar es Salaam. Profesa Ibrahim anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mkuu Mstaafu Othman Chande na kuwa jaji wa nane kushika wadhifa huo tangu nchi ipate uhuru huku akiwa Mtanzania wa sita. Wapili kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi
Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa Ibrahim Hamis Juma akisaini hati ya kiapo mara baada ya kuapishwa
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akitia saini hati ya kiapo cha Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa Ibrahimu Hamisi Juma baada ya kumuapisha
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya kiapo Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Profesa Ibrahimu Hamisi Juma
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza baada ya kumuapisha Jaji Mkuu wa Mahakama Tanzania Mhe. Profesa Ibrahimu Hamisi Juma leo
Jaji Mkuu wa Mahakama Tanzania Profesa Ibrahimu Hamisi Juma akizungumza baada ya kuapishwa leo
Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi akizungumza baada ya Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahimu Hamisi Juma kuapishwa
Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi (kushoto) akiteta jambo na Jaji Mkuu mstaafu Othman Chande (kulia) na Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju wakati wa hafla hiyo ya kuapishwa kwa Jaji Mkuu wa Tanzania
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya majaji waliohudhuria hafla ya kumuapisha Jaji Mkuu wa Tanzania
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Habari (MAELEZO) na Msemaji Mkuu wa Serikali Dk. Hassan Abbasi akifuatilia kwa makini hafla hiyo
Jaji Kiongozi Ferdinand Wambaliakiteta jambo na Jaji Mkuu Mstaafu Othman Chande (kulia) wakati wa hafla hiyo
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa hafla hiyo.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Jaji Mkuu Mstaafu Othman Chande baada ya kumuapisha Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahimu Hamisi Jum. Kulia ni Spika wa Bunge Job Ndugai
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akizungumz na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi wakati wa hafla hiyo
Rais Dk. John Magufuli akiwa na Jaji Mkuu na Spika wa Bunge wakati wa hafla hiyo
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan, Jaji Mkuu wa Tanzania Profesa Ibrahim Hamis Juma, Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Job Ndugai na Majaji mbalimbali, mwisho mwa hafla hiyo,leo Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Sunday, July 16, 2017
UMOJA WA VIJANA WA CCM VYUO NA VYUO VIKUU MKOA WA MWANZA WAKAKABIDHIWA VYETI NA NAIBU KATIBU MKUU CCM BARA
Sunday, July 16, 2017Mgeni Rasmi Katika Mahafali ya wahitumu wa Vyuo vikuu Mkoa wa Mwanza Ndugu Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Rodrick Mpogolo , Akiongozana na Daniel Zenda K.katibu Idara Vyuo na Vyuo Vikuu , Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndgugu Anthony Dialo, Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndg Raymond Mwalimu, Waheshimiwa Wabunge wa Ilemela na Nyamagana pamoja na viongozi wa secretariat ya Mkoa, Katibu wa CCM Nyamagana na viongozi mbali mbali wa Chama cha Mapinduzi, Makundi ya Kijamii, Machinga, wapiga debe, Mama Ntilie na wajasiliamali. Mahafali yaliyofanyika Ukumbi Rock City Mall.
Ndugu Mgeni Rasmi amewasihi sana wahitimu kuwa Wabunifu wa miradi za kuweza kujitegemea haswa katika Kilimo na Ufugaji, Mgeni Rasmi aliwakumbusha wahitimu kuenenda sawa na Imani ya Ccm kama ilivyoainishwa katika katiba ya CCM Ibara ya nne (4) na aliwataka wahitimu Wajiajiri(Blue colour Job) na kutumia Maarifa waliyonayo katika Jamii na kuondokana na dhana ya kuajiriwa.
Aliendelea kusisitiza Umuhimu wa Database yani taarifa za wahitimu wote zinaumuhimu sana kwa kutumikia chama cha Mapinduzi na Taifa kwa Ujumla.
Mahafali ya kwanza kubwa Mkoani wanafunzi/Makada walio hitimu 256 na washiriki walio hudhuria 612 wanachama.
Mahafali hiyo ilifana kwa kuanza Shughuli ya kijamii kutembelea kituo cha Watoto waliofanyiwa Ukatili(Foundation Karibu Tanzania) kaimu katibu Idara Vyuo na Vyuo Vikuu ndg Daniel Moses Zenda aliongoza Shughuli hiyo na kujionea namna Ukatili waliofanyiwa watoto hao. Pamoja na kushiriki na kutoka Mchango Ulioandaliwa na Wanafunzi wa Vyuo Vikuu.
Imetolewa na
Idara Vyuo na Vyuo Vikuu.

RAIS MAGUFULI NA MKEWE JANETH MAGUFULI WASHIRIKI IBADA YA JUMAPILI KATIKA PAROKIA BIKIRA MARIA CHATO
, July 16, 2017
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli pamoja na mke wake Mama Janeth Magufuli wakitoa sadaka wakati wa ibada ya jumapili katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo julai 16, 2017.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na Mkewe Janeth Magufuli wakisikiliza mahubiri toka kwa Padri Henry Mulinganisa wakati wa ibada ya jumapili katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo Julai 16 2017.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisisitiza jambo wakati wa ibada ya jumapili katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo Julai 16, 2017.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliyeshika kikapu cha sadaka akipokea sadaka toka kwa Mke wake Bi Janeth Magufuli wakati wa kuchangia ujenzi na upanuzi wa katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita, leo Julai 16, 2017.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli aliyeshika kikapu cha sadaka akipokea sadaka kutoka kwa waumini wakati wa kuchangia ujenzi na upanuzi wa katika kanisa la Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa ameshika kikapu chenye michango ya fedha zilizotolewa na waumini wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa hilo, leo Julai 16, 2017
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru mmoja wa waumini wa kanisa hilo ndugu Mwita Chacha mara baada ya kuchangia mifuko mitano ya saruji kwaaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita .
Mama Janeth Magufuli mke wa Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiahidi mchango wake wa ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akishuhudia mmoja wa waumini wa kanisa hilo ndugu Deogratius Ambrosi mwenye ulemavu wa mkono,akitoa mchango wake wa kiasi cha shilingi elfu tano kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimshukuru mmoja wa waumini wa kanisa hilo ndugu Deogratius Ambrosi mwenye ulemavu wa mkono,akitoa mchango wake wa kiasi cha shilingi elfu tano kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwashukuru waumini walioshiki kuchangia ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita,ambapo zilikusanywa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni kumi na tatu pamoja na ahadi mbalimbali za vikiwemo vifaa vya ujenzi.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa nje ya kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita, ambalo linaendelea kupanuliwa na kujengwa hapo akielekea kuwasalimia waumini walio kuwa nje ya kanisa na kuwaaga baada ya ibada.
Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiondoka kwenye kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita, mara baada ya ibada.
Katibu wa Rais Ndugu Ngusa Samike (kushoto) akikabidhi mchango wa Mhe Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli jumla ya shilingi milioni kumi kwaajili ya ujenzi na upanuzi wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita,
Waumini wa kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita wakiwa kwenye ibada.
Jengo la kanisa Katoliki la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita linaloendelea kupanuliwa na kujengwa
Waumini wa kanisa Katoliki la Bikira MariaParokia ya Chato Mkoani Geita wakitoka kwenye ibada ya jumapili




























































