Saturday, July 15, 2017

Watu wanaokunywa kahawa wanaishi miaka mingi: Utafiti

Rorya blog 5 hours ago

Ukikunywa vikombe vitatu vya kahawa kwa siku unaweza kuishi miaka mingi, kwa mujibu wa utafiti uliofanyiwa karibu watu nusu milioni kutoka nchi 10 za Ulaya. 

Utafiti huo uliochapishwa kwenye jarida na Annals of Internal Medicine, unasema kuwa unywaji wa kahawa unaweza kuongeza maisha ya mtu. 

Lakini wataalamau wanasema kuwa ni vigumu kusema kuwa ikiwa ni unywaji kahawa unachangia watu kuishi miaka mingi au ni maisha ya kiafya wanayoishi wanywaji kahawa. 

Watafiti kutoka shirika la Agency for Research on Cancer and Imperial College London, wanasema wamegundua kuwa unywaji wa kahawa nyingi unahusiana na hatari kidogo ya kufariki hasa kutokana na magonjwa ya moyo. 

Waliafikia uamuzi baada ya kuchunguza takwimu kutoka kwa watu walio na umri wa zaidi ya miaka 35 kutoka nchi 10 za Ulaya. 

Waliawauliza watu wakati wakianza utafiti kuhusu kiasi cha kahawa walikuwa wakinywa kisha wakaangali vifo vilivyotokea katika kipindi cha miaka 16. 

Lakini cha kuvunja moyo kwa wanywaji wa kahawa, ni kuwa ugunduzi huu haueleweki vyema. 

Kwa mfano haukuonyesha ni kipato cha kiwango gani wanywaji pombe hupata ikilinganishwa na wale wasiokunywa kahawa. 

Huenda ikawa labda watu walio na uwezo wa kununu vikombe vitatu vya kahawa kila siku wana pesa zaidi, na kwa njia moja au nyingine huwasaidia kulinda afya zao.  miaka mingi: Utafiti

Muungwana Blog · 5 hours ago

Ukikunywa vikombe vitatu vya kahawa kwa siku unaweza kuishi miaka mingi, kwa mujibu wa utafiti uliofanyiwa karibu watu nusu milioni kutoka nchi 10 za Ulaya. 

Utafiti huo uliochapishwa kwenye jarida na Annals of Internal Medicine, unasema kuwa unywaji wa kahawa unaweza kuongeza maisha ya mtu. 

Lakini wataalamau wanasema kuwa ni vigumu kusema kuwa ikiwa ni unywaji kahawa unachangia watu kuishi miaka mingi au ni maisha ya kiafya wanayoishi wanywaji kahawa. 

Watafiti kutoka shirika la Agency for Research on Cancer and Imperial College London, wanasema wamegundua kuwa unywaji wa kahawa nyingi unahusiana na hatari kidogo ya kufariki hasa kutokana na magonjwa ya moyo. 

Waliafikia uamuzi baada ya kuchunguza takwimu kutoka kwa watu walio na umri wa zaidi ya miaka 35 kutoka nchi 10 za Ulaya. 

Waliawauliza watu wakati wakianza utafiti kuhusu kiasi cha kahawa walikuwa wakinywa kisha wakaangali vifo vilivyotokea katika kipindi cha miaka 16. 


Lakini cha kuvunja moyo kwa wanywaji wa kahawa, ni kuwa ugunduzi huu haueleweki vyema. 

Kwa mfano haukuonyesha ni kipato cha kiwango gani wanywaji pombe hupata ikilinganishwa na wale wasiokunywa kahawa. 

Huenda ikawa labda watu walio na uwezo wa kununu vikombe vitatu vya kahawa kila siku wana pesa zaidi, na kwa njia moja au nyingine huwasaidia kulinda afya zao. 

Jaffo awatahadhalisha ma-Ded, na Ma-DC Kuhusu Utapeli

Rorya maendeleo Blog 1 hour ago


VIONGOZI wa kada mbalimbali nchini, wametahadharishwa kuwa makini na watu wanaofanya vitendo vya utapeli kwa kutumia majina na picha za viongozi wa juu, wakiwamo mawaziri ili kujipatia fedha.. 

Tahadhari hiyo ilitolewa jana mjini hapa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, (Tamisemi), Selemani Jafo, alipokuwa akifunga mafunzo ya viongozi hao kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa. 

Mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo ni ya awamu ya pili kutolewa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na ofisi ya Rais Tamisemi na yamejumuisha viongozi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa. 

Jafo alisema kumeibuka wimbi la utapeli wa kutumia majina ya viongozi kuwalaghai viongozi mbalimbali kwenye wilaya kutuma fedha. 

“Kumekuwapo na watu wanatumia picha na majina ya viongozi kutuma ujumbe mfupi wa kuwataka wakuu wa wilaya au mikoa na wakurugenzi kutuma fedha wakidai kuwa kiongozi fulani amepatwa na jambo fulani la dharura. Naomba mjiepushe na watu hawa kwa kuwa ni matapeli,” alisema Jafo. 

Alisema matapeli hao wamekuwa wakitumia majina ya viongozi wa ngazi za juu serikalini kwa madai kwa wanauguliwa au wamepata shida mbalimbali wawapo safarini jambo ambalo si kweli. 

“Nataka kuwapa angalizo kuweni makini. Kama mtu atakuwa na shida kama ni waziri atampigia katibu wake au atatumia nafasi yake kutoa taarifa ili kupatiwa huduma lakini si kwa kupigiwa simu au kutuma ujumbe mfupi,” alisema Jafo. 

Aidha, aliwataka kusimamia mipango ya maendeleo iliyopo kwenye bajeti ya mwaka huu wa fedha na kuhimiza wafanye kazi kwa manufaa ya Taifa na siyo kwa manufaa yao. 

Jafo aliwataka wakatumie mafunzo hayo kama chachu ya kuwafanya kuwa na weledi mkubwa zaidi tofauti na ilivyo kuwa hapo awali. 

Nabu Waziri Jafo aliwataka wakurugenzi kutozalisha madeni ya watumishi katika halmashauri zao. 

“Hakuna sababu yoyote ya halmashauri kuwa na madeni ambayo hayana msingi na msiwahamishe watumishi bila kuwa na maandalizi ya malipo,” alisema. 

Naye, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Uongozi, Denis Rweyemamu, alisema mafunzo yanalenga kuwajengea uwezo ili kufanya kazi kwa malengo ya maendeleo. 

Alibainisha kuwa licha ya viongozi hao kufanya kazi vizuri, bado walitakiwa kupata mafunzo ili kuongeza weledi katika utendaji kazi.

Serikali yagoma kupokea Misaada yenye Masharti haya

Rorya maendeleo Blog. 1 hour ago



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan amesema Taifa halipo tayari hata kidogo kupokea misaada yenye masharti ambayo haiendani na mila na desturi za Kitanzania. 

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Ireland Mary Robinson pamoja na Mwanzilishi wa Taasisi ya Graca Machel, Craca Machel pamoja na ujumbe walioambatana nao Ikulu- Jijini Dar es Salaam. 

Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa kuna baadhi ya wafadhili wanaisaidia Serikali katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na bajeti vizuri sana na bila masharti mabaya lakini kuna baadhi ya wafadhili wanaonyesha wazi kuwa wanataka Serikali ikubali masharti yao ambayo yanaenda kinyume na maadili ya taifa kitu ambacho hakiwezekani. 

Amesema kutokana na changamoto hiyo Serikali itaendelea kusimamia maadili ya Taifa ipasavyo na imeweka mipango na mikakati mizuri kwa ajili ya kuongeza mapato yake ya ndani ili kuondokana na utegemezi kutoka kwa baadhi ya wafadhili ambao baadhi yao wanaahidi kuchangia bajeti kuu ya Serikali lakini mwisho hawafanyi hivyo. 

Kuhusu Sekta ya afya, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Serikali imeongeza maradufu bajeti yake kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018 katika sekta ya afya ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya kwa viwango vinavyotakiwa nchini. 

Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa Ireland Mary Robinson pamoja na Mwanzilishi wa Taasisi ya Kimataifa ya Graca Machel, Craca Machel waipongeza Serikali kwa jitihada inazozifanya katika uimarishaji wa sekta ya afya nchini na wameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha huduma za afya nchini zinaendelea kuboreshwa ipasavyo.

Rooney asepa na Wachezaji wanne wa Bongo

Rorya maendeleo

Mkurugenzi wa Uendeshaji wa SportPesa Tanzania, Abbas Tarimba amesema wanatarajia kuandaa mpango maalumu wa kuwasaidia wachezaji wa hapa nchini angalau wanne kila mwaka kwenda England kwa ajili ya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa. 

“Tunataka soka la Tanzania ilipige hatua ili siku moja na sisi tuwe na wachezaji wanaocheza  katika Ligi Kuu England. 

 “Tunajipanga ili tuweze kuleta maskauti hapa nchini kwa ajili ya kuangalia wachezaji na ikiwezekana angalau kila mwaka Watanzania wanne waweze kwenda England kwa ajili kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa ili siku moja tuweze kuwaona wakipambana na akina Rooney katika ligi kuu ya nchi hiyo,” alisema Tarimba.

Friday, July 14, 2017

Kesi ya Mbowe na DC yaanza kusikilizwa

Rorya maendeleo· 2 hours ago

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Moshi, jana ilianza kusikiliza kesi inayomkabili Mkuu wa Wilaya (DC) ya Hai, Gelasius Byakanwa. 

Kiongozi huyo amefunguliwa kesi na Kampuni ya Kilimanjaro Veggies Ltd, inayomilikiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe. 

Katika shauri hilo, kampuni hiyo inamlalamikia mkuu huyo wa wilaya kwa kushiriki kuharibu shamba la mboga mboga linalomilikiwa na Mbowe katika Kijiji cha Nshara wilayani Hai, Mkoa wa Kilimajnaro. 

Wakili wa upande wa utetezi anayemwakilisha mkuu huyo wa wilaya, Modestus Njau, aliiomba mahakama hiyo kukubali ombi la 

kumjumuisha katika shauri hilo Mwanasheria Mkuu wa Serikali kutokana na umuhimu wake. 

Pamoja na hayo, wakati kesi hiyo inayosikilizwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Aishael Sumari ikiendelea, upande huo wa utetezi uliiomba 

mahakama hiyo iahirishe shauri hilo ili kupata muda mzuri wa kupitia madai ya mlalamikaji. 

Akizungumza mahakamani hapo, wakili huyo alidai kuna umuhimu wa kumjumuisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kesi 

hiyo kwa kuwa mshtakiwa ni mkuu wa wilaya na anashtakiwa kutokana na majukumu ya Serikali aliyokuwa akiyatekeleza. 

Kwa mujibu wa Wakili Njau, sheria ya Tamisemi ya mwaka 1997, sehemu ya 14, kifungu kidogo cha kwanza na cha pili, kinataja kazi za mkuu wa wilaya na majukumu yake na kwamba majukumu hayo ndiyo yaliyosababisha afikishwe mahakamani. 

Kutokana na maombi hayo, Wakili wa Kampuni ya Uwakili ya D’Souza & co ya jijini Arusha inayoiwakilisha Kampuni ya Mbowe, Meirad Souza, alikubaliana na maombi hayo, lakini akataka yawasilishwe kwa maandishi. 

Akitoa uamuzi wake, Jaji Sumari alimtaka mdaiwa kuleta majibu pinzani ya kiapo, Julai 27 mwaka huu na mlalamikaji arudishe majibu Agosti 3, 

mwaka huu. 

Pamoja na hayo, Jaji Sumari aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 14, mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa. 

Juni 30 mwaka huu, Kampuni ya Uwakili ya D’ Souza & Co ya jijini Arusha, kwa niaba ya Kampuni ya Kilimanjaro Veggies Ltd, 

inayomilikiwa na Mbowe, ilimfungulia kesi mkuu huyo wa Wilaya ya Hai na kumtaka alipe fidia ya zaidi ya Sh milioni 549.3. 

Katika kesi hiyo namba 20/2017 yenye maombi madogo namba 51/2017, mdai anaomba zuio la muda liweze kutolewa dhidi ya mkuu huyo wa wilaya ili asifanye chochote katika shamba lililoharibiwa mazao lenye ukubwa wa ekari 2.7.

ACACIA kulipa mirabaha iliowekwa katika sheria mpya za madini

ACACIA kulipa mirabaha iliowekwa katika sheria mpya za madini

.Kampuni inayomiliki Makampuni ya Uchimbaji wa Madini ya ACACIA imesema italipa mirabaha iliowekwa katika sheria mpya za madini. 

Sheria mpya ya madini inawataka wawekezaji katka sekta hiyo kulipa asilimia 6 ya mirabaha ikiwa ni ongezeko la asilimia 2 zilizokuwepo awali, ambapo asilimia 1 ni kwaajili ya usafirishaji kwenda nje. 

Monday, June 19, 2017

Victor makotieno atema cheche IPTL

Uamuzi wa ICSID kuhusu IPTL mshindi Ni Tanzania

Septemba 12, 2016 Mahakama ya Usuluhishi wa migogoro ya uwekezaji iliwasilisha rasmi maamuzi yake Kwa pande zilizokuwa kwenye mgogoro kuhusu mradi wa kufua umeme Nchini, IPTL. Mahakama hiyo iliamuru kwamba Benki ya Standard Chartered ya Hongo Kong ( SCB-HK ) ilipwe dola za Kimarekani 148 milioni sawa na Fedha za Kitanzania shilingi 320 bilioni. Mahakama hiyo Pia imeamuru kuwa kuchotwa Kwa Fedha kutoka akaunti maalumu ya TEGETA Escrow hakukuondoa Haki ya ya Benki ya SCB-HK kwenye kampuni ya IPTL na hivyo kisheria kwamba Benki hiyo Kwa sasa ndio mwenye uhalali wa shughuli zote za IPTL.

Ilinichukua Siku takribani 2 kusoma na kusoma tena tuzo hii (Award ) ili kuweza kuielewa haswa maana yake Kwa Nchi yetu. Ikumbukwe kwamba niliongoza Kamati ya Bunge iliyoagiza uchunguzi wa sakata la TEGETA Escrow Account na kuandaa Taarifa Maalumu ya Kamati ya PAC iliyosomwa na kukubaliwa rasmi na Bunge na kupitisha maazimio 8 yaliyopaswa kutekelezwa na Serikali. Baada ya kuisoma Kwa kina Tuzo hiyo ya ICSID nilichoona Ni kwamba masuala Yale Yale ambayo PAC iliyafafanua Bungeni Mwezi Novemba mwaka 2014 ndio hayo hayo yaliyopelekea tuzo hiyo. Kwa maana hiyo Ni kwamba iwapo Serikali ingetekeleza Maazimio ya Bunge yote Leo hii tungekuwa kwenye nafasi nzuri sana ya kulimaliza suala Hilo kabisa na kuachana kabisa na mgogoro huu ambao unanyonya Fedha za Watanzania.

Kuna masuala makuu 2 ambayo yakieleweka suala la kashfa ya IPTL litakuwa limeeleweka na maamuzi yanaweza kufanyika kumalizana nalo.

1. baada ya mbia ya kampuni ya Mechmar kufilisika nchini Malaysia, Ni Nani mwenye Haki na Mali za IPTL?
2. Tozo ya malipo ya umeme uliozalishwa na IPTL ilizidishwa? 
Kwenye Taarifa ya Kamati ya PAC tulionyesha Kwa vielelezo na ushahidi kwamba kampuni ya PAP haikuwa ina umiliki wa kihalali wa asilimia 70 ya Hisa za IPTL. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alionyesha dhahiri kuwa vyeti vya Hisa ( shares certificates ) za kampuni ya Mechmar kwenye IPTL walikuwa nazo Benki ya SCB-HK Kama dhamana ya mkopo waliowapa IPTL. CAG aliziona hati hizo Kwa macho yake kwenye uchunguzi wake ambao ndio uliotumika na PAC kufikia maazimio 8 ya Bunge.

Vile vile Kamati ya PAC ilionyesha Kwa ushahidi kuwa PAP hawakufuata sheria za Tanzania katika kumiliki IPTL ikiwemo kwamba walikwepa kodi kupitia kampuni iliyoitwa PiperLink ya British Virgin Island. TRA walikiri mbele ya Kamati kuwa wakati Mahakama Kuu inatamka kuwa PAP wapewe ' masuala ( affairs ) ya IPTL ) hawakuwa na uhalali wa kufanya Biashara Tanzania kwani hawakuwa wamepewa kibali na Kamishna Mkuu wa Kodi cha kuthibitisha utwaaji wao wa kampuni ya IPTL. Hivyo Kamati ililiambia Bunge kuwa PAP ni matapeli wa Kimataifa waliopiga ganzi Mfumo wa Serikali ya Tanzania Kwa kutumia rushwa na hivyo kuhalalishiwa umiliki wa IPTL ili kuchota Fedha zilizokuwa kwenye akaunti ya TEGETA Escrow Benki Kuu ya Tanzania.

Hata Gavana wa Benki Kuu alipowaomba PAP uhalali wa wao kumiliki IPTL walichotoa ni kitu kinachoitwa Deed of Assignment badala ya shares certificates. Watanzania watakumbuka kuwa Deed of Assignments ndizo zilizotumika kuiba Benki Kuu kwenye wizi wa EPA mwaka 2004-2005. Jambo la kushangaza Ni kwamba karatasi hiyo ya kugushi ilikubaliwa na hivyo Bwana Harbinder Singh Seth wa PAP akaruhusiwa kuchota mabilioni ya Fedha kutoka Benki Kuu ya Tanzania. Kwa mujibu wa Mwanasheria wa TANESCO Bwana Richard Rweyongeza TANESCO waliilipa PAP $245m Sawa na shilingi 530 bilioni. Itakumbukwa kuwa wakati PAC inasoma Taarifa yake Fedha hizo zilikuwa tshs 306 bilioni tu.

Katika tuzo yake ICSID imethibitisha kuwa PAP hakuwa mmiliki wa IPTL na hivyo alilipwa Fedha za TEGETA Escrow kimakosa. Hoja hii imethibitisha Hoja ya PAC na Bunge la Tanzania ambayo ilipingwa vikali na Serikali ya wakati huo ambayo iligeuka mtetezi wa PAP. Uamuzi wa ICSID kwamba TANESCO wailipe SCB-HK unathibitisha kuwa PAP alipewa Fedha za TEGETA escrow kitapeli.

Baada ya kumaliza hoja hiyo twende Hoja ya pili; je Hata Kama PAP wangekuwa Ni Wamiliki halali wa IPTL walilipwa ziada?

Itakumbukwa kwamba PAC ililiambia Bunge kuwa mgawo wa Fedha ulipaswa kusubiri kukokotoa kanuni za mgawo ambazo ziliamriwa na Mahakama hiyo ya ICSID. Hoja kubwa ya PAC ilikuwa ' Ni Kwanini tulifanya haraka kutoa Fedha kabla ya Uamuzi wa kiwango gani kilipwe? '. Hoja hii ndio iliyochagiza kuwa mule ndani ya TEGETA escrow kulikuwa na Fedha za umma. Uamuzi wa kukokotoa ukatolewa Mwezi Februari mwaka 2014 lakini katika mjadala mzima wa sakata la TEGETA escrow Serikali ilikataa kata kata kutekeleza Uamuzi huu. Hata kwenye Hoja za TANESCO mahakamani huko hawakuwa kabisa na Hoja kulinda Uamuzi ule. Hata hivyo ICSID imeamua kuwa tulikuwa tunaliwa Kwa kulipa tozo kubwa zaidi ya kiwango tulichopaswa kulipwa. Hii maana yake Ni kwamba Hata kwenye hizo za wizi tuliilipa PAP zaidi ya tulichopaswa kuwalipa.
Katika magazeti ya Leo wakili aliyeiwakilisha TANESCO anasema " tulibishania Hoja ya kulipa Kwa viwango vya zamani ikaamuriwa hesabu zifanyike upya Mahakama iliamuru hesabu zifanyike upya Kwa kutumia mkopo wa wana Hisa ". Hii ndio Hoja ambayo PAC iliijenga Kwa muda mrefu na kubezwa na Serikali ndani ya Bunge Kwa mbwembwe zote. Wakili wa TANESCO anaendelea " kutokana na hesabu hizo gharama ilikuwa chini. IPTL ililipwa zaidi hivyo inatakiwa kurejesha Dola za Marekani zaidi ya milioni 100 Kwa TANESCO ".

Hii ndio ilikuwa Hoja ya PAC ambayo ilitokana na maagizo ya CAG kwamba TANESCO wakae chini na SCB-HK kupiga hesabu upya. Hoja hii ilikataliwa na Serikali na TANESCO wenyewe ilipotolewa na PAC lakini Leo mwanasheria wa TANESCO aliyeiwakilisha TANESCO katika Mahakama ya Usuluhishi ya ICSID anakiri tuliwalipa zaidi IPTL.

Jambo la kushangaza Ni kwamba, licha ya ushindi huu mkubwa Kwa Tanzania na TANESCO wanasheria wanataka tukate rufaa. Magazeti ya Serikali ya Dailynews na habari leo ndio yameongoza na habari hiyo. Ikumbukwe kuwa magazeti hayo ndio Siku zote yamekuwa yakiitetea pap na Bwana Seth. Ni dhahiri kuwa ama wanasheria wanataka waendelee kulipwa Fedha kwenye kesi au kuna shinikizo kubwa kutoka Kwa wanaofadika na mchezo huu wa kutapeli ili waendelee kufisadi Nchi. Uamuzi huu wa ICSID unatuweka kwenye nafasi nzuri sana ya kulimaliza kabisa suala la IPTL kwani umetuonyesha kuwa;
1)Kwa miaka yote ya uwepo wa IPTL tumekuwa tunapigwa Kwa kulipa capacity charges Mara mbili ya kiwango tulichopaswa kulipa
2)Tulitapeliwa na Bwana Seth kupitia kampuni ya PAP ambayo Wamiliki wake wengine 50% mpaka sasa hawajulikani Ni kina Nani licha ya kuwajua Kwa jina la Simba Trusts ya Australia.  

Wakati wanasheria na baadhi ya maofisa wa Serikali waliofadika na mgawo wa TEGETA escrow wanataka kukata rufaa wanajua kuwa maamuzi ya ICSID hayana rufaa Kwa mujibu wa Ibara ya 53 ya mkataba wa ICSID ( no appeal except those provided for in the ICSID Convention ). Hadhi  yake Ni Sawa na maamuzi ya Mahakama ya juu kabisa ya Tanzania Kwa mujibu wa Ibara ya 54 ya mkataba wa ICSID ( convention ). Hata hivyo maamuzi hayo yanaweza kuombewa kufutwa Kwa kutumia Ibara ya 52(2) Kwa sababu maalumu ambazo Ni

a). Baraza la Usuluhishi halikuundwa kisheria ( properly constituted ). Ijulikane kuwa Baraza hili huteuliwa na washiriki wa kesi. SCB-HK waliteua msuluhishi wao, TANESCO waliteua wao na Kwa pamoja wakateua Rais wa Baraza. Hivyo TANESCO hawana Hoja maana Hata msuluhishi waliteua wao kakubaliana na maamuzi haya ya tuzo hii.
b). Kwamba Baraza lilienda nje ya mamlaka yake. TANESCO walishiriki mwanzo mwisho na hawakuwa na malalamiko kuhusu Hilo wanawezaje kuwa na malalamiko sasa. Hata msuluhishi wao kakubali maamuzi haya.
c). Kwamba kulikuwa na rushwa kwenye kufikia maamuzi haya. TANESCO wanaweza kutoa ushahidi Kama Hata msuluhishi waliyemteua wao alihongwa!
d) kwamba tuzo haina sababu za kufikia maamuzi haya. Kwa walioisoma tuzo hii wanajua kuwa sababu zipo kinagaubaga kabisa.

Kwa maoni yangu kutaka kesi iendelee Ni kutaka kulinda maslahi ya wanaofadika na suala zima la IPTL. Suala hili sasa liishe. Nchi imeshaliwa sana. Itoshe.

Ushauri wangu Kwa Serikali Ni Kama ifuatavyo

1. Kutekeleza tuzo hii ya ICSID bila kusita
2. Kuiamrisha kampuni ya PAP kurejesha Fedha zote za ziada ilizolipwa kutoka akaunti ya TEGETA escrow. Kwa mujibu wa tuzo hii Ni jumla ya tshs 202 bilioni
3. Kuitaka kampuni ya PAP kuilipa Benki ya SCB-HK kutokana na hati iliyowasilisha Benki Kuu kwamba madai yeyote yakitokea katika IPTL PAP ndio watalipa ( indemnity ).
4. Kuchunguza na kuishtaki PAP na Bwana Harbinder Singh Seth Kwa utapeli na utakatishaji wa Fedha Kwa mujibu wa sheria za Tanzania
5. Kuchunguza na kuwashitaki maofisa wote wa Serikali walioshirikiana na Seth kuchota Fedha Benki Kuu
6. Kuilipisha faini Benki ya StanBic Tanzania Kwa kushiriki kwenye vitendo vya kutakatisha Fedha kufuatia miamala ya TEGETA escrow
7. Kufunga kabisa suala la IPTL Kwa kuvunja mkataba na kuitwaa mitambo Kwa mujibu wa sheria za Tanzania

Natumai kuwa watu wenye nafasi za Uongozi wa umma ambao maamuzi Yao yamefikisha Nchi hapa watachutama na kuondoka katika Uongozi wa umma. Tumefikishwa hapa na wizi na tamaa za watu madalali wa matapeli. Ninaamini kuwa Rais John Pombe Magufuli hatakubali Nchi hii kuendelea kupigwa na matapeli.

Victor makotieno
Rorya
19/06/ 2017