Tuesday, May 17, 2016

Rais Mugabe awa babu Zimbabwe

Rais Mugabe awa babu Zimbabwe

  • Saa 3 zilizopita
Image copyright Reuters
Image caption Mugabe ameongoza Zimbabwe tangu 1980
Kiongozi wa muda mrefu wa Zimbabwe Robert Mugabe, 92, amekuwa babu rasmi.
Hi ni baada ya bintiye wa pekee Bona Chikore kujifungua mtoto mvulana katika hospitali moja nje ya nchi hiyo.
Bi Chikore alijifungua mtoto huyo mwezi uliopita, gazeti la serikali la Herald limeripoti.
Image copyright RIA Novosti
Bw Mugabe amesema mkewe Grace kwa sasa yuko pamoja nab inti huyo wao na mjukuu wao na kwamba watarejea Zimbabwe mwezi ujao.

Libya kupewa silaha kupambana na IS

Libya kupewa silaha kupambana na IS

  • Saa 5 zilizopita
Image caption Viongozi wakijumuika katika mazungumzo ya Libya
Nchi 25 ikiwemo Marekani zimekubaliana kuipa silaha serikali ya Libya kwa lengo la kuiwezesha kukabiliana na wanamgambo wa IS wanaoendelea kuisumbua nchi hiyo.
Muungano wa kimataifa umesema kuwa utalegeza vikwazo vya silaha vya Umoja wa Mataifa juu ya Libya kutoa silaha kwa vikosi vinavyounga mkono serikali mpya ya Tripoli.
Waziri mkuu wa Libya Fayez al-Sarraj, amesema kuwa IS wamekuwa kikwazo kikubwa sana kwa nchi yake na msaada huo wa kimataifa utakuwa muhimu katika kupambana na ugaidi kwa mafanikio.
Nchi hizo tano ambazo ni wanachama wa kudumu wa baraza la usalama la umoja wa mataifa walifikia makubaliano hayo baada ya mazungumzo mjini Vienna.Libya imekumbwa na machafuko tokea kuangushwa kwa kanali Gaddafi mwaka 2011.

Uh, Barack Obama is totally in the new ‘Mr. Robot’ trailer

Uh, Barack Obama is totally in the new ‘Mr. Robot’ trailer

USA
The trailer for the second season of the USA Network’s acclaimed psychological thriller Mr. Robot was released today. Besides looking as deliciously suspenseful as we’ve come to expect from the hacker drama, this clip has a secret weapon: An apparent cameo from one Barack Obama, an up-and-coming actor you may be familiar with from his previous role as president of the United States of America.
Obama appears on a TV screen in the midst of what looks like a garden-variety press conference. His comments are generic as you’d expect—at least, they start off that way. “There hasn’t been anything like this in the past,” Obama says. “This is going to be affecting our economy in ways that are extraordinarily significant.”
This statement sounds like it could have been repurposed from any old speech precisely because it was. In fact, those two sentences are stitched together from the president’s end-of-the-year remarks to the White House press corps in December 2014. In that context, the first line referred to normalizing relations with Cuba and the second—more in line with the themes of Mr. Robot—to cyber attacks.
But from there, the voice of Obama gets awfully specific. “The FBI announced today that Tyrell Wellick and fsociety engaged in this attack,” he says, seemingly commenting directly on the events of the show’s first season. Uh…
Former E Corp executive and forever sociopath Tyrell Wellick (Martin Wallström) is a Mr. Robot character, and fsociety is the Coney Island-based hacker group led by the titular Mr. Robot (Christian Slater). Both, of course, are fictional, and very, very unlikely to have ever been mentioned in POTUS stock footage that somebody in the production office happened to find lying around.
Golden Globe or no Golden Globe, it would be an unbelievable coup if the series managed to recruit our Commander in Chief, seasoned TV star though he may be, to record some dialogue. But if not Obama, that’s one hell of a voice actor: Who? How? What?
Then again, with a little movie magic, the 1997 sci-fi flick Contact borrowed real-life footage of Bill Clinton discussing a rock from Mars and made it sound like the then President was talking about the extraterrestrial signals at the heart of the plot. I wouldn’t put anything past Mr. Robot, particularly not a feat of editing.
We’ve reached out to the USA Network in the hopes of getting to the bottom of this presidential mystery. Stay tuned.
Mr. Robot returns July 13 at 9 p.m. ET on the USA Network.

US, other powers want to arm Libyan government

US, other powers want to arm Libyan government

by rorya.

VIENNA (AP) — In a move fraught with risk, the United States and other world powers said Monday they would supply Libya's internationally recognized government with weapons to counter the Islamic State and other militant groups gaining footholds in the chaos-wracked country's lawless regions.
Aiming at once to shore up the fragile government, and prevent Islamic State fighters and rival militias from further gains, the U.S., the four other permanent U.N. Security Council members and more than 15 other nations said they would approve exemptions to a United Nations arms embargo to allow military sales and aid to Libya's so-called "Government of National Accord."
In a joint communique, the nations said that while the broader embargo will remain in place, they are "ready to respond to the Libyan government's requests for training and equipping" government forces.
E.U foreign policy chief Federica Mogherini arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (AP Photo/Ronald Zak)
E.U foreign policy chief Federica Mogherini arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (AP Photo/Ronald Zak)
"We will fully support these efforts while continuing to reinforce the UN arms embargo," the communique said.
With support from all five permanent members of the U.N. Security Council, the plan is unlikely to face significant opposition from any quarter.
The communique was issued at the end of the talks that gathered U.S. Secretary of State John Kerry and top officials from more than 20 other nations to discuss ways to strengthen Libya's fledgling government. The aim is to give the internationally recognized administration more muscle in fighting Islamic State radicals and end its rivalry with a group to the east claiming legitimacy.
The step will boost the government's efforts to consolidate power and regain control over Libyan state institutions like the central bank and national oil company. However, it also comes with risks, not least of which is that the arms may be captured or otherwise taken by the Islamic State or other groups.
Kerry called the plan "a delicate balance."
"But we are all of us here today supportive of the fact that if you have a legitimate government and that legitimate government is fighting terrorism, that legitimate government should not be victimized by (the embargo)," he told reporters.
Libyan Premier Fayez al-Sarraj said his government would soon submit a weapons wish list to the Security Council for approval.
"We have a major challenge ahead of us," in fighting extremists, he said. "We urge the international community to assist us."
Before the meeting, German Foreign Minister Frank-Walter Steinmeier outlined the high stakes at hand.
"The key question is whether Libya remains a place where terrorism, criminal human smuggling and instability continue to expand, or if we are able, together with the government of national unity to recover stability," he told reporters.
The challenges are daunting.
Libya descended into chaos after the toppling and death of Moammar Gaddafi five years ago and soon turned into a battleground of rival militias battling for powers. More recently, the power vacuum has allowed Islamic State radicals to expand their presence, giving them a potential base in a country separated from Europe only by a relatively small stretch of the Mediterranean Sea.
Also worrying for Europe is the potential threat of a mass influx of refugees amassing in Libya, now that the earlier route from Turkey into Greece has been essentially shut down. British Foreign Secretary David Hammond said his government had received a request from the Libyan government to bolster its Coast Guard — a project "which will address Libyan concerns about smuggling and insecurity on their border but will also address European concerns about illegal migration."
In Libya, meanwhile, the U.N.-established presidency council on Monday effectively gave the go-ahead for 18 government ministers to start work, even though they have not received backing from the parliament.
The council was created under a U.N.-brokered unity deal struck in December to reconcile Libya's many political divisions. It won the support of a former powerbase in the country's capital, Tripoli, but failed to secure a vote of confidence by the country's internationally recognized parliament, based in Tobruk, a city in eastern Libya.
The U.N. deal also created the internationally recognized government, through a de facto Cabinet to administer the country under Prime Minister-designate Fayez Serraj and the 18 ministers will answer to him.
Divisions in theTobruk parliament between boycotters and supporters of the new government have prevented the house from reaching a quorum to endorse the council.
U.S. Secretary of State John Kerry , center, , Italian Foreign Minister Paolo Gentiloni , left, and U.N. Libya envoy Martin Kobler  attend the ministerial me...
U.S. Secretary of State John Kerry , center, , Italian Foreign Minister Paolo Gentiloni , left, and U.N. Libya envoy Martin Kobler attend the ministerial meeting on Libya in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (Leonhard Foeger/Pool Photo via AP)
U.S. Secretary of State John Kerry , center, , Italian Foreign Minister Paolo Gentiloni , left, and U.N. Libya envoy Martin Kobler  attend the ministerial me...
U.S. Secretary of State John Kerry , center, , Italian Foreign Minister Paolo Gentiloni , left, and U.N. Libya envoy Martin Kobler attend the ministerial meeting on Libya in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (Leonhard Foeger/Pool Photo via AP)
British Foreign Secretary Philip Hammond, center, arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (AP Photo/Ronald Zak)
British Foreign Secretary Philip Hammond, center, arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (AP Photo/Ronald Zak)
U.S. Secretary of State John Kerry ,  left, arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (AP Photo/Ronald Zak)
U.S. Secretary of State John Kerry , left, arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. (AP Photo/Ronald Zak)
German Foreign Minister Frank-Walter Steinmeier arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016.  As top diplomats begin meeting on bringing ...
German Foreign Minister Frank-Walter Steinmeier arrives for Libya talks in Vienna, Austria, Monday May 16, 2016. As top diplomats begin meeting on bringing peace to Libya, Germany's foreign minister says it is too early to say whether talks will succeed in moving toward that goal.(AP Photo/Ronald Zak)

Sunday, May 1, 2016

Mwasomola na somo la sauti kuu.

SAUTI KUU AU KILIO KIKUU CHA MWISHO

imeandaliwa na Mch. Kenani Mwasomola, Uwakili - SHC

Fungu kuu: Ufunuo 18:1 – 5. “Baada ya hayo naliona Malaika mwingine,
akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi
ikaangazwa kwa utukufu wake. Akalia kwa sauti kuu, umeanguka
maskani ya mashetani, na ngome ya kila roho mchafu, na ngome ya
kila ndege mchafu mwenye kuchukiza, kwa kuwa mataifa yote
yamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake, na wafalme wa
nchi wamezini naye, na wafanya biashara wa nchi wamepata mali
kwa nguvu za kiburi chake”
Utangulizi: Neno malaika, ambalo kwa kiyunani ni “angelosi”
humaanisha mjumbe au taarishi. Neon hili limetumiwa sana katika
kitabu cha Ufunuo. Mahala pengine limetumiwa kumaanisha malaika
wa Mungu watokao juu. Hawa nao ni wajumbe wa Mungu waletao
habari njema kutoka juu mbinguni kwa wanadamu. Lakini pia
wanadamu wanaomwamini Yesu na kupeleka injili ya wokovu kwa
wanadamu wenzao nao hujulikana kama Malaika – wajumbe wa
Bwana.
MALAIKA WA KILIO KIKUU: katika Ufunuo 14:8 ujumbe wa malaika wa
pili unasikika “---- umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio
mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya
ghadhabu ya uasherati wake.
Je Babeli anayetajwa kwamba umeanguka ni nini? Babeli kwangu
kabisa humaanisha machafuko. Babeli ni kanisa la kiulimwengu na
lililoenea ulimwenguni kote. Babeli imeyafanya mataifa yote kunywa
mvinyo ya ghadhabu ya uasherati wake ambayo ni mafundisho ya
uongo yaliyo kinyume na neno la Mungu. Hivyo Babeli huwakilisha
kanisa la kidunia tu.
Uriah Smith, The prophecies of Daniel end the Revelation
(Washington, DC: Review and Herald Publishing Association, 1994) pg.
646 – 7.
Babeli ule mji mkubwa unaundwa na makundi matatu. Hivyo dini
kubwa ya dunia hii zinaweza kupangwa katika vichwa vitatu:
1. ya kwanza na ya zamani sana na iliyoenea sana ni upagani (ukafiri
yaani ushenzi) unawakilishwa na joka.
2. Ya pili ni uasi mkubwa wa upapa, unawakilishwa na mnyama.
3. Ya tatu ni mabinti(makanisa yanayofuata uasi wa upapa) au wazao
wa kutoka kanisa la Rumi ya kiroho, yakiwakilishwa na mnyama
mwenye pembe mbili, ingawaje hiyo haichukui yote.
Vita, mateso, unafuatisha namna ya dunia hii, mtindo wa kidini
ibada ya (mali), kutafuta anasa, na kudumisha kila kosa la kanisa
katoliki, kwa huzuni hudhihirisha makanisa ya Kiprotestant kuwa
sehemu muhimu ya Babeli mkuu 2. Ujumbe wa unaanguka kwa Babeli
ulitolewa kwa mara ya kwanza mnamo 1844 na wanamarejeo watu
walioamini kuwa Yesu angerudi mnamo 22 Oktoba 1844. Huu ujumbe
ulikuwa ni onyo kwa watu ambao walikanusha na kupinga ujumbe wa
marejeo ya Yesu Kristo. Ujumbe huo utarudiwa tena kwa usahihi
kabisa na malaika mwingine ambaye awafuata wale malaika watatu
wa Ufunuo 14:6 – 12. ujumbe wa malaika wa Ufunuo 18:1 – 5
utatolewa kwa nguvu ya mvua ya masika Roho Mtakatifu
atakayemwagwa kwa wingi juu ya watu wa Mungu walio waaminifu
katika kufuata neno la Mungu na wenye imani ya Yesu.
Watu wa Mungu, wakiwa wamejazwa Roho Mtakatifu (Mvua ya
masika) watasonga mbele kwa nguvu wakitoa mwito kwa watu
walioko katika Babeli ili watoke kurudi wasije wakashiriki
maangamizo yake yaliyo ya hakika. [Uriah Smith, The Prophecies of
Daniel and the Revelation, P. 647.]
Yohana anaandika kisha nikasikia sauti nyingine kutoka
mbinguni ikisema, tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi
zake, wala msipokee mapigo yake. Kwa maana dhambi zake zimefika
hata mbinguni, na Mungu amekumbuka maovu yake (Ufunuo 18:4 –
5) “---- ujumbe wa malaika wa tatu utatangazwa kwa uweza mkuu na
wale wanaotoa onyo la mwisho dhidi ya mnyama na sanamu
yake” (8T 118). Matangazo hayo, yakiungana na ujumbe wa malaika
wa tatu yanakuwa sehemu ya onyo la mwisho litakalotolewa kwa
wakazi wa dunia hii (GC 604). “WATU WA Mungu ambao bado
watakuwa Babeli wataitwa ili wajitenge na ushirika wake. Ujumbe
huu ndio wa mwisho ambao utapata kutolewa kwa ulimwengu” (GC
390)
Watu maelfu kwa maelfu watatoka kutoka katika Babeli na kujiunga
na watu wa Mungu na Mungu atatia muhuri wake juu yao.
MAIGIZO YA SHETANI KABLA YA KUTIMIZWA KWA UFUNUO 18:1
Mjumbe wa Mungu, Ellen G. White anasema ya kwamba, Adui
wa roho za watu anataka kuzuia kazi hii, na kabla ya wakati wa
vuguvugu kama hilo kuja, atajitahidi kulizuia kwa kuleta uamsho wa
bandia. Katika yale makanisa ambayo naweza kuyaleta chini ya uwezo
wake wa madanyanyo atafanya ionekane kuwa mbaraka pekee wa
Mungu unamwagwa juu yao, kutaonekana kila kinachodhaniwa kuwa
ni mwamko mkubwa wa mambo ya kidini. Makutano ya watu
watashangilia wakisema kwamba Mungu anatenda maajabu kwa ajili
yao, wakati kazi hiyo ni ya roho yule mwingine. Akiwa amejificha
chini ya vazi la dini, shetani atajaribu kuueneza ushawishi wake katika
ulimwengu wote wa Kikristo (GC 464)
Kila siku watu wanasikia na pengine hata kushuhudia maajabu
yanayofanywa kwa jina la Yesu lakini kwa undani wake hasa maajabu
hayo yanafanywa kwa uwezo wa adui Ibilisi. Katika siku hizi za
mwisho shetani, kupitia watumishi wake, atafanya ishara kubwa za
uponyaji na hata kufanya moto kushuka kutoka mbinguni uje juu ya
nchi mbele ya wanadamu. Naye atawakosesha wale wakaao juu ya
nchi kwa ishara zile alizopewa kuzifanaya (Ufunuo 13:13,14). Watu
wengi watakoseshwa kwa ishara hizo na maajabu hayo. Lakini watu
wa Mungu kamwe hawatashibishwa. Daima wao watakumbuka, hata
ishara kubwa na maajabu yasiyo ya kawaida yatakapotendeka mbele
ya macho yao, neno lao ni moja tu, imeandikwa na waende kwa
sheria na ushuhuda, ikiwa hawasemi sawasawa na neno hili, kama
mtu anayefanya ishara za uponyaji, unenaji wa lugha, kufufua watu au
hata kushusha moto kutoka juu mbinguni, hashiki amri za Mungu
na wala hana ushuhuda wa Yesu ambao ni Roho ya unabii(Ufunuo
19:10) huyo mtu hakutumwa na Mungu na roho itendayo kazi ndani
yake siyo ya Mungu. Watu wa Mungu washikao amri za Mungu
(Ufunuo 14:12)nao watafanya ishara na miujiza. Lakini daima
watakumbuka kuwa imani yao haikujengwa juu ya miujiza na
maajabu bali imani yao imejengwa juu ya msingi wa mitume na
manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni.
(Waefeso 2:20)
TUWEZAJE KUPAMBANUA KATI YA UAMSHO BANDIA WA SHETANI NA SAUTI
KUU?
Mjumbe wa Mungu, anaweka bayana ya kwamba katika
uamsho bandia, kuna msisimuko wa kihisia kuchanganya ukweli na
uongo, ambavyo vimekusudiwa kuwapotosha watu. Hata hivyo,
hakuna haja kwa yeyote kudanganyika. Katika nuru ya neno la Mungu
si vigumu wanapodharau ushuhuda wa Biblia, wakigeukia na
kuziacha zile kweli zilizo dhahiri na zenye kuupima moyo na ambazo
zinahitaji kujikana nafsi na kuukataa kabisa ulimwengu, hapo ndipo
tunapoweza kuwa na uhakika ya kwamba mbaraka wa Mungu,
haujatolewa. Na kwa kanuni ile aliyoitoa Kristo mwenyewe,
mtawambua kwa matunda yao (Mathayo 7: 16),ni dhahiri kwamba
vuguvugu hilo siyo kazi ya Roho wa Mungu (GC 464, 465)
Je Ni lini ambapo anguko la Babeli (Ufunuo 18:2) litakuwa
limetimilika hata Ufunuo 18:2 liweze kuhubiriwa kama uliotimia
kabisa? “ uliowanywesha mataifa, yote mvivyo wa ghadhabu ya
uasherati wake” (Ufunuo 14:8) Mafundisho ya uongo. Jambo hilo
linafanyikaje? Kwa kuwalazimisha watu kuikubali sabato ya uongo(8T
94) Jumapili ndiyo sabato ya uongo. Ni mpaka hapo hali hiyo
itakapofikiwa na muungano wa kanisa lna ulimwengu
utakapokamilika anguko la Babeli litakapokuwa limekamilika. Badiliko
ni la kuendelea, na utimizo kamili wa ufunuo 14:8 bado uko siku za
usoni (GC 390).
Kupitishwa kwa amri ya Jumapili kutakuwa ndiyo mwanzo wa
taabu na mateso.Lakini “mwanzoni mwa wakati wa taabu, tulijazwa
na Roho Mtakatifu tulipoondoka kwenda kuitangaza Sabato kwa
ukamilifu zaidi” (EW 33, NA 85). “Sabato hiyo ya uongo italazimishwa
kwa sheria ya ukandamizaji. Shetani na malaika zake wako macho
sana, tena wanashughulika kwa nguvu sana -----. Lakini wakati shetani
atakapofanya kazi kwa maajabu yake ya uongo, ndipo utakapotimizwa
wakati uliotabiriwa katika Ufunuo, na malaika yule mwenye mamlaka
kuu atakayeitangaza dunia yote kwa utukufu wake, atatangaza anguko
la Babeli, na kuwaita watu wa Mungu walioko huko watoke (7BC 985,
RH 13/12/1892).
SAUTI KUU ITAFANANA NA PENTEKOSTE.
Kazi hiyo itafanana na ile ya siku ya pentekoste. Kama vile
mvua ya vuli iliyotolewa kwa kumwaga Roho Mtakatifu mwanzoni
mwa kazi ya injili ili kusababisha kuchipua kwa mbegu zile za
thamani, ndivyo “ Mvua ya masika itakavyotolewa mwishoni ili
kukomaza mavuno” (GC 611)…“Kumwagwa kwa Roho katika siku za
mitume ilikuwa ni mvua ya vuli, na matokeo yake yalikuwa ya
utukufu sana. Lakini mvua ya masika itakuwa nyingi zaidi” (Ev 701).
Je, watoto wa Mungu ambao bado watakuwa Babeli
wataupokea mwito wa sauti kuu? Jawabu ni ndiyo. Mjumbe wa
Mungu Ellen White anasema, Roho zilizokuwa zimetawanyika katika
mashirika yote ya kidini ziliitikia mwito na zile zilizokuwa za thamani
ziliharakishwa kutoka katika makanisa yakwenda kuangamizwa, kama
vile Lutu alivyoharakishwa kutoka Sodoma kabla ya maangamizi yake
(EW 279). Hakuna chochote kitakachoweza kuwazuia wabakie
Babeli. Mahusiano ya kifamilia, mahusiano ya kikanisa, sasa hayana
uwezo wowote wa kuwazuia. Ukweli ni wa thamani zaidi kuliko
mengine yote.Bila kujali mawakala walioungana dhidi ya ukweli, idadi
kubwa ya watu, watachukua msimamo wao upande wa Bwana. (GC
612).
WAADVENTISTA WASABATO AMBAO HAWAJAONGOKA.
Jambo la kusikitisha, Waadventista wa Sabato ambao
hawajaongoka hawatatambua sauti kuu na wataipinga kazi
hiyo. White anasema kuwa “kutakuwa na udhihirisho wa ajabu wa
uweza wa Mungu katika makanisa yetu, lakini uweza huo hautawajia
wale ambao hawajajinyenyekeza wenyewe mbele za Bwana, na
kuifungua mioyo yao kwa maungamo na toba katika udhihirisho wa
uweza unaoiangaza dunia yote kwa utukufu wake, wao wataona tu
kuwa ni mila fulani ambacho katika upofu wao watafikiria kuwa ni
cha hatari, kitu fulani kitakachoamsha hofu zao, nao watajidhatiti
kuupinga kwa kuwa Bwana hafanyi kazi yake kulingana na matarajio
na mawazo yao, basi, wataipinga kazi hiyo. Watasema “kwa nini sisi
tusiweze kumjua Roho wa Mungu wakati tumekuwa kazini kwa miaka
mingi sana?” RH 7/11/1918…. “Dhoruba inapozidi kukaribia, kundi
kubwa la wale wanaodai kuwa na imani katika ujumbe wa malaika
wa tatu lakini ambao hawakutakaswa kwa kuitii ile kweli, wataziacha
nafasi zao na kujiunga katika safu za wapinzani” (GC 608)
Huu ndio wakati wa kila mmoja kuchukua msimamo thabiti
kuwa upande wa Bwana. Wale wanongojea wakati fulani wa pekee
ambamo watategemea tabia zao kugeuka ghafla na kuwa kama Kristo,
wakati huo hawataupata. Leo hii ndivyo nafsi na wakati wa kupata
mvua ya vuli (Roho Mtakatifu wa kwanza) tayari kwa kupokea mvua
ya masika yaani Roho Mtakatifu atakayemwagwa bila kipimo wakati
wa mwisho na atayewawezesha malaika wa Ufunuo 18:1 – 5 kupeleka
ujumbe wa onyo la mwisho kwa kishindo kikubwa sana.
“Wakati uweza wa Mungu utakapounganishwa na juhudi za
binadamu, kazi itaenea kama moto katika nyasi kavu zilizokatwa
Mungu atatumia mawakala ambao asili yao mwanadamu hataweza
kuifahamu, malaika watafanya kazi ambayo wanadamu wangeweza
kupata mibaraka ya kutimiza, kama wasingepuuzia kuitikia madai ya
Mungu” (RH 15/12/1885)
Mambo makuu ya kufanya ili kujiandaa kwa wakati huo wa mwisho:-
1. Soma neno la Mungu (Biblia) kila siku
2. Omba bila kukoma. Uwe na maombi ya mnyororo katika maisha
yako yote.
3. Fanya kazi ya kuihubiri Injili waweza kuhubiri kwa njia ya kupeleka
vitabu, sauti ya unabii, Biblia yasema, masomo ya mgunduzi,
mahubiri ya hadhara, kuonana kuombea wagonjwa hospitalini na
majumbani n.k. Mungu atatungoja sisi kama watu wake tuweze
kuifanya kazi yake kwa mali, nguvu, na akili zetu.
Wito: ni nani basi ajitoaye kwa moyo ili ajiweke wakfu kwa Bwana?
(1Nyakati 29:5)

Friday, April 29, 2016

TAARIFA YA MKAGUZI WA TAWI LA CHUO KIKUU CHA IRINGA.

UTANGULIZI.
taarifa ya ofisi ya mkaguzi wa tawi la Chuo kikuu cha IRINGA.
Wapendwa katika bwana. Napenda kutoa shukrani Kwa Bwana wetu yesu kwani ndie kiongozi na mkaguzi wa matendo yetu yoto hapa duniani na wakili wetu siku ya ukumu kule Juu.
1. Glory madiwa(mkaguzi komfrenci) Kwa kunifundisha kazi na kunivumilia katika maswali yangu yoto. Kwakweli alijitoa kunisaidia na Mungu atakubariki. Nitumie pia fursa hii kuwashukuru mwanatawi letu Kwa ushirkiano wenu ndani ya mwaka huu wa 2015-2016 Kwa umoja na mshikamano wenu.
Katika safari hii yakwenda Kwa bwana tukumbuke kwamba njia yetu ni nyembamba hivyo kama tulikosana tusameane kwani hayo ndiyo miba, mawe, yanayopatikana ndani ya njia hiyo.

UTENDAJI WA KAZI NDANI YA MWAKA 2015-2016.
- tumefanikiwa kufanya kazi Kwa pamoja na vyongozi japo walikua baathi tu.
- ofisi ya mkaguzi (CAG wakanisa) tumefanikiwa kukagua taarifa zote za fedha za tawi Bila kupoteza hata shilingi ya tawi nakufanya tawi letu kupewa Hati Safi kwani kila robo taarifa ya mkaguzi ilikua ikibaini changamoto na siyo matumizi mabaya ya pesa. Kitu iliyofanya kila robo mkaguzi kutuma Hati Safi Kwa kiongozi Wa Kanda.
- ofisi ya mkaguzi ilifanya kazi masaa 24 na kupelekea kila kiongozi kuwajibika japo wengine walifanya mambo Yao Kwa kuificha ofisi ya CAG.
CHANGAMOTO.
1. vyongozi kutumia madaraka Vibaya toka mwenyekiti, katibu, mtunza azina. Mfano. Kutoa pesa njee ya tawi Bila kuwasiliana na ofisi ya CAG.
2. Kutokutoa taarifa za utendaji Kwa kila idara kama mawasiliano, na kuperekea vyombo au vifaa kupotea, kuaribia na tawi kufanya matumizi yasiyo yalazima kama kununua na kutengeneza vifaa vya tawi.
3. Vyongozi kutokufahamu mipaka ya madaraka Yao na kufanya wengine kuwa vyongozi hewa bila kufanya kazi. Mfano m/kiti kupata taarifa na kutuma moja Kwa moja Kwa wanachama bila kujali kazi ya kiongozi Wa mawasiliano na kufanya huvujifu wa mishingi ya uongozi yani (Lider ship ethics).
MWISHO.
Baba Mungu wabariki vyongozi wapia.
By. Baraka Boniphace.
CAG wa tawi letu. 

Tuesday, April 26, 2016

Kimenuka bungeni - Nondo zilizomo kwenye report ya CAG::

::Kimenuka bungeni - Nondo zilizomo kwenye report ya CAG::

=> Ulaji na uzembe vinatajwa kubeba sehemu kubwa ya ripoti hii.

=> Misamaha ya kodi 2014/15 ni asilimia 2 ya pato la taifa kinyume cha asilimia 1

=> Halmashauri 40 hivi ndo zenye hati safi kati ya halmashauri zaidi ya 1

=> Bidhaa a bilioni 9 za kupelekwa nje ziliuzwa hapa hapa nchini. Upigaji huo wa ukwepaji kodi.

=> Bidhaa za bilioni 89 za nje hakuna ushahidi kama zilienda Rwanda, Burundi na Uganda.

=> Rufaa za kodi nyingi mno zimedoda mahakamani na hivyo kuikosesha serikali kodi

=> Deni la Taifa hadi Juni 2015 lilifikia trilioni 33.5. Ndani ya mwaka mmoja lilikua kwa trilioni 7!

=> Malipo kwa deni kwa mwaka ni trilioni 4.

=> Deni na mishahara inamaliza mapato yote ya taifa. CAG anahoji, tutapata wapi pesa za maendeleo?

=> CAG Anataka maduka ya fedha za kigeni yadhibitiwe

=> Vyama vya siasa, kimoja tu kimewasilisha hesabu. Vyama 21 bado, Msajili afiatilie. Hajakitaja chama kilichowasilisha

=> Mishahara hewa katika Taasisi za umma 16 ni Shilingi bilioni 390. Mishahara ambayo haikulipwa na haikurejeshwa hazina ni bilioni 2

=> Sh. Milioni 700 za makato ya watumishi kwa Katavi na Kilimanjaro hayakuwasilishwa kwenye mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

=> Sh. Milioni 827 za vifaa vya upigaji kura zilitumika kwa kazi isiyo na tija katika Uchaguzi 2015

=> Nakala 158,003 za Katiba Pendekezwa hazikusambazwa kwa walengwa wakati wa mchakato wa Katiba Mpya

=> Manunuzi yenye thamani ya Sh. Bilioni 27 yalifanywa na Mashirika ya Umma bila ushindani

=> Cheti cha uendeshaji ATC kimeisha muda tangu 2010. ATC ina Wafanyakazi wengi kuliko kazi zilizopo

=> CAG ataka UDA irejeshwe serikalini. Mwenyekiti wa Bodi ya UDA, Idd Simba aliwekewa sh. milioni 320 ktk akaunti yake binafsi.

=> Kampuni ya SAAFI inadaiwa Sh. bilioni 17. Hii ni ya mwanasiasa mkongwe, Mzindakaya.
MPEKUZI

Tanzania Entertainment News,Politics News ,Celebrity Gossip and Live Updates

HomeEnglish NewsDisclaimerAdvertise Here

Tuesday, April 26, 2016

Ripoti ya CAG Yaanika 'Madudu' Kibao Serikalini

Wakati Rais John Magufuli akipambana dhidi ya ufisadi, uzembe na ukwepaji kodi na uovu mwingine dhidi ya mali za umma, ripoti mpya ya ukaguzi iliyotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali inaonyesha ana kazi kubwa zaidi kupata ushindi kwenye vita hiyo. 

Ripoti hiyo ya mwaka 2014/ 2015 iliyowasilishwa bungeni jana na CAG Mussa Juma Assad imeibua uozo zaidi kwenye halmashauri, taasisi za Serikali na mashirika ya umma, ikibainisha kuwa nchi ina tatizo kubwa zaidi ya watu ambao wamekuwa wakishughulikiwa na Serikali ya Awamu ya Tano. 

 

Ripoti hiyo ya pili ya Professa Assad tangu ateuliwe kushika nafasi hiyo mwaka juzi, imegusa taasisi zilizowahi kuwa chini ya Rais John Magufuli na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako na Balozi Asha Rose Migiro, ambaye alikuwa Waziri wa Sheria na Katiba. 

 

Ripoti hiyo pia inaonyesha ufisadi katika ununuzi na uingiaji mikataba uliofanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), matumizi yasiyo ya lazima kwenye Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Afya, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jeshi la Wananchi, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na mkoa wa Tabora. 

 

Pia ripoti hiyo imebainisha kuwa mapendekezo mengi ambayo CAG amekuwa akiyatoa kwa takribani miaka saba sasa, hayatekelezwi. 

 

Katika ripoti hiyo, CAG anaonyesha dosari kwenye utendaji wa Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme (Temesa), na Wakala wa Barabara (Tanroads), taasisi zilizo chini ya Wizara ya Ujenzi ambayo wakati huo ilikuwa ikioongozwa na Dk Magufuli. 

 

Profesa Ndalichako alikuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), wakati NEC imeguswa na ripoti hiyo katika suala la mchakato wa kuandika Katiba upya ulioongozwa na Wizara ya Katiba na Sheria. 

 

Ripoti hiyo ya Profesa Assad pia imebainisha kuwa Deni la Taifa, ambalo hutokana na fedha zinazopowa kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kugharimia matumizi ya Serikali, limekuwa kwa tofauti ya Sh7 trilioni. 

 

Tangu aingie madarakani Novemba 5 mwaka jana, Dk Magufuli amekuwa akitumia ripoti zilizopita za CAG kusimamisha kazi au kutengua uteuzi wa watumishi wa umma wanaotuhumiwa kujihusisha na ufisadi, lakini amekuwa akikosolewa kuwa hajaweka mfumo wa kukabiliana na hali hiyo. 

 

Katika ripoti hiyo, CAG anasema Temesa ilinunua kivuko chenye kasi ndogo kuliko ilivyotarajiwa na hadi ulipokuwa unafanyika ukaguzi Agosti 2015, chombo hicho kilikuwa hakifanyi kazi kwa zaidi ya mwaka. 

 

“Kuhusu dosari katika ununuzi wa kivuko chenye thamani ya Sh7,916,955,000, Wizara ya Ujenzi kupitia Wakala wa Umeme, mitambo na ufundi (Temesa) iliingia mkatabana M/s Johs.Gram-Hanssen Bergensgade 10, DK 2100 Copenhagen Oe Denmark wa ununuzi wa kivuko cha Dar es Salaam –Bagamoyo chenye thamani ya Dola za Marekani 4,980,000 bila Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT),” anasema CAG. 

 

“Dosari zifuatazo zilibainika katika manunuzi hayo. Kasi ya kivuko haikuzingatia matakwa ya mnunuzi.  Ripoti ya mtaalamu wa ukaguzi ilibainisha kwamba kiwango cha juu na chini cha kasi ya kivuko wakati wa majaribio kilikuwa na kiwango kati ya knots 19.45 na knots 17.25 kinyume na makubaliano yaliyoainishwa kwenye mkataba wa kasi ya kiwango cha 20,” anafafanua.

 

“Pili kivuko kilikabidhiwa bila hati ya makabidhiano Novemba 17, 2014 baada ya ucheleweshwaji wa siku 16; Pia nilibaini kwamba mpaka wakati wa ukaguzi, Agosti 2015, hati ya makabidhiano ilikuwa haijatolewa na mzabuni.” 

Ununuzi wa feri hiyo uliwahi kuzua sakata bungeni huku wabunge wa upinzani wakilalamika kwamba kilikuwa bomu kwani kinatumia zaidi ya saa tatu kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo badala ya dakika 45 za gari. 

 

Eneo jingine lililoguswa na CAG ni la malipo yaliyofanywa na Tanroads kwa makandarasi waliomaliza kazi zao. Kwamba moja ya matatizo makubwa ya taasisi hiyo ni udhaifu katika menejimenti. 

 

“Wakala wa Barabara (Tanroads) iliingia mikataba mbalimbali ya ujenzi wa barabara na madaraja. 

 

"Wakati wa ukaguzi nilibaini kwamba baadhi ya mikataba haikukamilika kwa muda uliopangwa kutokana na kuchelewa kwa ulipaji wa fedha. 

  

"Pia, nilibaini kwamba ucheleweshwajiwa malipo ya kati ya mikataba 16 ulisababisha ulipaji wa riba kiasi cha Sh 5,616,652,022 na Dola za Marekani 686,174.86,” alisisitiza CAG. 

 

Profesa Assad amezungumzia pia ukaguzi maalumu alioufanya kuhakiki fedha zilizowahi kutolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa taasisi mbalimbali zilizoko chini yake. 

 

Ukaguzi huo ulifanywa kutokana na ombi lililowasilishwa na katibu wa Bunge kwa barua yenye Kumb. NaCBC.155/188/01/26 ya Desemba 19, 2013. 

Bunge lilitaka kujua kama fedha zilizotolewa na wizara hiyo kwenda idara na taasisi zilizo chini yake zilipokewa na kutumiwa na wahusika kama ilivyopangwa. 

 

Katika ukaguzi huo, CAG alibaini kasoro katika vitabu vya akaunti za fedha vya Necta mwaka 2010, Sekretarieti ya Elimu ya Jumuiya ya Madola, Chuo Kikuu Huria (OUT), na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (Adem). 

 

“Udanganyifu wa malipo ya Sh185,350,000 yaliyolipwa Necta. Aprili 2010 kiasi cha 185,350,000 kilitumwa Necta kama matumizi ya kawaida. Wakati wa ukaguzi ilibainika kuwa kiasi hiki cha fedha hakikuandikwa kwenye vitabu vya uhasibu vya Necta. Hata hivyo, ilibainika kuwa stakabadhi ya mapokezi ya fedha hizo iliyotolewa na watumishi wasio waaminifu wa Necta ilikuwa ya kugushi,” anasema. 

 

“Kuhusu fedha zilizopelekwa OUT ni kwamba kati ya mwaka 2009/2010 Wizara ilihamisha Sh90,000,000 kwenda Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, ni kiasi cha Sh40,734,000 ambacho kilipokewa huku Sh49,266,000 hakijulikani. 

 

“Pia katika mwaka wa fedha 2010/2011 Wizara ilipeleka OUT Sh10,486,252,913 lakini ni Sh10,427,109,020 tu zinazoonekana kwenye vitabu huku Sh59,143,893 zikiwa hazimo kwenye vitabu.” 

Vilevile, CAG amesema katika ukaguzi huo Sh188, 838,528 zilizopelekwa Adem mwaka 2009/2010 zimeyeyuka. Mwaka huo Wizara ilipeleka Sh712,798,788 kwa taasisi hiyo, lakini vitabu vinaonyesha Sh523,960,260 zilipokewa na kurekodiwa, huku Sh188, 838,528 zikikosekana kwenye vitabu. 

 

Mbali ya CAG kuonyesha madudu katika matumizi ya fedha, pia ameonyesha matumizi mabaya ya Sh7,080 milioni katika mchakato wa uchapaji Katiba Inayopendekezwa. 

 

“Katika ukaguzi wangu nilibaini kuwa Wizara ya Katiba na Sheria ilipokea fedha kiasi cha Sh7,125 milioni kwa ajili ya kulipia gharama za kuchapisha vitabu vya Katiba Inayopendekezwa. 

"Kutokana na ufinyu wa muda, Wizara iliomba na kupewa kibali na Wakala wa Huduma za Manunuzi Serikalini kufanya manunuzi kwa njia ya dharura kupitia barua yenye kumbukumbu Na CAD.124/318/01/25 ya Desemba 11, 2014,” anasema CAG. 

 

“Katika ukaguzi wangu nilibaini vitabu vya katiba vilipokelewa kabla ya kuingia mkataba. Nilibaini kuwa mkataba ulisainiwa Februari 2, 2015, lakini vitabu vya katiba vilipokelewa Januari 26, 2015.” 

Ukaguzi uliofanywa Oktoba Mosi, 2015 umebaini kuwa nakala 158,003 za Katiba Inayopendekezwa zenye thamani ya Sh559,330,620 bado viko stoo au havijatumwa kwa wananchi ili vitumike kwa uhamasishaji. 

 

“Kwa hiyo, haikuwa rahisi kujua kama thamani halisi ya fedha ilipatikana na lini vitabu hivi vitasambazwa kwa walengwa. Pia, ilibainika kuwa vitabu hivyo havikujumuishwa kwenye Taarifa za Fedha za Mwaka husika,” anasema. 

 

Katika ripoti hiyo ya mwaka 2015/16, CAG Assad anasema ukaguzi wake umebaini matumizi ya mabilioni ya fedha katika ununuzi wa vitu visivyokuwa vya lazima au bila kuonyesha ushahidi wa malipo husika. 

 

Alibainisha matumizi ya zaidi ya Sh53 bilioni zilizotumiwa na taasisi sita pamoja na Sekretarieti mbili za mikoa katika mambo ambayo hayakuwa ya lazima, kama faini za kuchelewa kulipa kodi ya pango. 

 

Taasisi hizo ni Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Afya, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi na Mkoa wa Tabora. 

 

CAG Assad amebainisha matumizi ya ziada ya Sh109,722, 539 kwa ajili ya ununuzi wa gari aina ya Toyota Land Cruiser VX V8 kwa Sh297.5 milioni kutoka kampuni ya Toyota (T) badala ya kutumia mfumo wa ununuzi wa pamoja ambao ungefanya gari hilo lipatikane kwa Sh187.8 milioni. 

 

Alisema katika kipindi hicho, wizara 17, balozi mbili na sekretarieti za mikoa 11 zilitumia zaidi ya Sh11.3 bilioni bila kuwapo vielelezo vyovyote, hivyo kusababisha ashindwe kujua uhalali wa malipo hayo. 

==> Kwa taarifa zaidi, pitia  ripoti hizi za CAG

 

1. Ripoti ya Jumla ya Serikali Kuu 2014/2015

2.Ripoti ya Jumla ya ufanisi na Uchunguzi 2014/2015

3. Ripoti ya Jumla ya Mashirika ya Umma 2014/2015

4. Ripoti ya Jumla ya Miradi ya Maendeleo 2014/2015

5. Ripoti ya Jumla ya Serikali za Mitaa 2014/2015

 

==

Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya Mpekuzi Blogkwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka

Tupe Maoni Yako( Matusi Hapana )

› Halmashauri 47 tu zilizopata Hati zinazoridhisha

1.Arusha DC 2.Makambako TC 3.Butiama DC 4.Kahama TC 5.Arusha CC 6.Wanging’ombe DC 7.Kyela DC 8.Ushetu DC 9.Monduli DC 10.Buhigwe DC 11.Busokelo Dc 12.Msalala DC 13.Bagamoyo DC 14.Kakonko DC 15.Kilombero DC 16.Bariadi TC 17.Kibaha DC 18.Uvinza Dc 19.Kilosa DC 20.Itilima DC 21.Kibaha TC 22.Moshi MC 23.Morogoro MC 24.Busega DC 25.Temeke MC 26.Siha DC 27.Gairo DC 28.Singida MC 29.Dar es Salaam CC 30.Lindi MC 31.Ilemela MC 32.Ikungi DC 33.Kinondoni MC 34.Mbulu DC 35.Nyang’hwale DC 36.Mkalama DC 37.Chemba DC 38.Simanjiro DC 39.Mbogwe DC 40.Bumbuli DC 41.Mufindi DC 42.Kiteto DC 43.Mlele DC 44.Kaliua DC 45.Iringa DC 46.Tarime TC 47.Nsimbo DC

Halmashauri 105 zilizopata Hati zenye Mashaka

1.Meru DC 2.Kongwa DC 3.Bukoba MC 4.Kilwa DC 5.Ngorongoro DC 6.Mpwapwa DC 7.Muleba DC 8.Lindi DC 9.Kisarawe DC 10.Dodoma MC 11.Karagwe DC 12.Liwale DC 13.Mafia DC 14.Iringa MC 15.Kyerwa DC 16.Nachingwea DC 17.Mkuranga DC 18.Kilolo DC 19.Kibondo DC 20.Ruangwa DC 21.Rufiji/Utete DC 22.Ludewa DC 23.Kigoma DC 24.Babati DC 25.Ilala MC 26.Njombe DC 27.Moshi DC 28.Hanang’ DC 29.Chamwino DC 30.Njombe TC 31.Mwanga DC 32.Babati TC 33.Kondoa DC 34.Makete DC 35.Rombo DC 36.Serengeti DC 37.Bahi DC 38.Biharamulo DC 39.Same DC 40.Musoma DC 41.Rorya DC 42.Ngara DC 43.Magu DC 44.Bunda DC 45.Tarime DC 46.Missenyi DC 47.Misungwi DC 48.Musoma MC 49.Mbeya DC 50.Ulanga DC 51.Ukerewe DC 52.Mpanda TC 53.Rungwe DC 54.Morogoro DC 55.Geita TC 56.Mpanda DC 57.Chunya DC 58.Mvomero DC 59.Geita DC 60.Tunduru DC 61.Mbeya CC 62.Masasi TC 63.Bukombe DC 64.Songea DC 65.Mbozi DC 66.Masasi DC 67.Chato DC 68.Nyasa DC 69.Ileje DC 70.Mtwara DC 71.Sumbawanga DC 72.Shinyanga DC 73.Mbarali DC 74.Newala DC 75.Nkasi DC 76.Shinyanga MC 77.Momba Dc 78.Tandahimba DC 79.Sumbawanga MC 80.Kishapu DC 81.Meatu DC 82.Nanyumbu DC 83.Korogwe DC 84.Maswa DC 85.Bariadi DC 86.Mtwara MC 87.Korogwe TC 88.Nzega DC 89.Manyoni DC 90.Mkinga DC 91.Kilindi DC 92.Sikonge DC 93.Singida DC 94.Lushoto DC 95.Igunga DC 96.Tabora DC 97.Pangani DC 98.Muheza DC 99.Urambo DC 100.Tabora MC 101.Tanga CC 102.Handeni DC 103.Karatu DC 104.Hai DC 105.Kigoma/Ujiji MC

Halmashauri 3 zilizopata Hati chafu

1. Karatu DC 2. Hai DC 3. Kigoma/Ujiji MC

Halmashauri 1 iliyopata Hati Mbaya

Tunduma Town Council

· Hawa walificha vitabu 79 vya mapato

· Walificha hati za malipo(voucher) zenye thamani ya SHS.178,511,580

· Malipo ya SHS.17,158,500 hayakuwa na viambatanisho

· Hawakuandaa vitabu vya hesabu

Home

View web version