Kutokana na malalamiko hayo, TFF imewaita wagombea wote wa ngazi ya juu wa KIFA wakiwamo viongozi waliochaguliwa katika uchaguzi huo kuhudhuria kikao cha Kamati ya Uchaguzi ya shirikisho kitakachofanyika kesho Jumamosi Juni 18, 2016 saa 3.00 asubuhi.
Pia, imewaita viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sambamba na Kamati za Uchaguzi za DRFA kadhalika ile ya KIFA ambazo zilisimamia uchaguzi huo ambao ulifanyika kwa mara ya pili mwishoni mwa wiki baada ya ule wa kwanza kuahirishwa mwezi uliopita.
No comments:
Post a Comment