Friday, April 29, 2016

TAARIFA YA MKAGUZI WA TAWI LA CHUO KIKUU CHA IRINGA.

UTANGULIZI.
taarifa ya ofisi ya mkaguzi wa tawi la Chuo kikuu cha IRINGA.
Wapendwa katika bwana. Napenda kutoa shukrani Kwa Bwana wetu yesu kwani ndie kiongozi na mkaguzi wa matendo yetu yoto hapa duniani na wakili wetu siku ya ukumu kule Juu.
1. Glory madiwa(mkaguzi komfrenci) Kwa kunifundisha kazi na kunivumilia katika maswali yangu yoto. Kwakweli alijitoa kunisaidia na Mungu atakubariki. Nitumie pia fursa hii kuwashukuru mwanatawi letu Kwa ushirkiano wenu ndani ya mwaka huu wa 2015-2016 Kwa umoja na mshikamano wenu.
Katika safari hii yakwenda Kwa bwana tukumbuke kwamba njia yetu ni nyembamba hivyo kama tulikosana tusameane kwani hayo ndiyo miba, mawe, yanayopatikana ndani ya njia hiyo.

UTENDAJI WA KAZI NDANI YA MWAKA 2015-2016.
- tumefanikiwa kufanya kazi Kwa pamoja na vyongozi japo walikua baathi tu.
- ofisi ya mkaguzi (CAG wakanisa) tumefanikiwa kukagua taarifa zote za fedha za tawi Bila kupoteza hata shilingi ya tawi nakufanya tawi letu kupewa Hati Safi kwani kila robo taarifa ya mkaguzi ilikua ikibaini changamoto na siyo matumizi mabaya ya pesa. Kitu iliyofanya kila robo mkaguzi kutuma Hati Safi Kwa kiongozi Wa Kanda.
- ofisi ya mkaguzi ilifanya kazi masaa 24 na kupelekea kila kiongozi kuwajibika japo wengine walifanya mambo Yao Kwa kuificha ofisi ya CAG.
CHANGAMOTO.
1. vyongozi kutumia madaraka Vibaya toka mwenyekiti, katibu, mtunza azina. Mfano. Kutoa pesa njee ya tawi Bila kuwasiliana na ofisi ya CAG.
2. Kutokutoa taarifa za utendaji Kwa kila idara kama mawasiliano, na kuperekea vyombo au vifaa kupotea, kuaribia na tawi kufanya matumizi yasiyo yalazima kama kununua na kutengeneza vifaa vya tawi.
3. Vyongozi kutokufahamu mipaka ya madaraka Yao na kufanya wengine kuwa vyongozi hewa bila kufanya kazi. Mfano m/kiti kupata taarifa na kutuma moja Kwa moja Kwa wanachama bila kujali kazi ya kiongozi Wa mawasiliano na kufanya huvujifu wa mishingi ya uongozi yani (Lider ship ethics).
MWISHO.
Baba Mungu wabariki vyongozi wapia.
By. Baraka Boniphace.
CAG wa tawi letu. 

No comments:

Post a Comment