Baadhi ya Wateja wa Kampuni ya Simu Ya Tigo wakiwa katika foleni kwa ajili ya kuhakiki simu zao zoezi linaloendelea kwa ushirikiano baina ya makampuni ya simu na TCRA leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya watoa huduma wa Tigo wakitoa huduma kwa wateja wao wakati wa kampeni ya kuhakiki simu kama ni Bandi au Orijino leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Mauzo wa 4G kutoka Tigo Anthony Assenga akisikiliza maoni ya wateja waliotembelea banda la tigo wakati wa kampeni ya kuhakiki simu kama ni Bandi au Orijino leo jijini Dar es Salaam.
Meneja Mauzo wa 4G kutoka Tigo Anthony Assenga akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu muitikio wa wananchi katika zoezi la kuhakiki simu kama ni Bandi au Orijino leo jijini Dar es Slaam.
Watoa huduma wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano Tanzania (TCRA – CCC) wakitoa huduma kwa wateja wakati wa kampeni ya kuhakiki simu leo jijini Dar es Salaam.
No comments:
Post a Comment