Wednesday, May 18, 2016

Liverpool, Sevilla zatinga fainali ya UEFA Europe League

Liverpool, Sevilla zatinga fainali ya UEFA Europe
League
Michezo miwili ya marudiano ya Ligi ya Vilabu Barani Ulaya (UEFA
Europe League) imechezwa usiku wa Alhamisi ambapo vilabu vya
Liverpool ya Uingereza na Sevilla ya Hispania wamefuzu kucheza
mchezo wa fainali.
Liverpool ilikuwa mwenyeji wa Villarreal ambapo iliibuka na ushindi wa
goli 3-0, magoli ya Liverpool yakifungwa na Bruno Soriano ambaye
alijifunga dk. 7, Daniel Strurridge dk. 63 na Adam Lallana dk. 81 hivyo
kufuzu kwa ushindi wa goli 3-1.
Mchezo mwingine ilikuwa ni Sevilla ambayo ilikuwa mwenyeji wa
Shakhtar Donetsk na Sevilla kuibuka na ushindi wa goli 3-1, magoli ya
Sevilla yalifungwa na Kevin Gameiro dk. 9, 47 na Mariano dk. 59 na
goli la kufutia machozi la Shakhtar Donetsk likifungwa na Eduardo na
hivyo kufuzu kwa ushindi wa goli 5-3.
Baada ya matokeo hayo, Liverpool na Sevilla zitapambana katika
mchezo wa fainali.

No comments:

Post a Comment