Friday, June 17, 2016

KILELE CHA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA CHAFANYIKA MVOMERO MKOANI MOROGORO



New Picture (11)Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga akihutubia wananachi wa mkoa wa Morogoro  waliohudhuria kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyoandaliwa na Mkoa wa Morogoro katika shule ya Msingi Kigugu, wilaya ya Mvomero
New Picture (12)Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga, katikati ni Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mhe. Betty Mkwasa na kulia ni Bibi Magreth wakipokea maelezo ya mratibu wa chanjo Mvomero kabla ya uzinduzi wa matone ya chanjo kwa watoto wa kata ya Kigugu wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika iliyofanyika shule ya Msingi Kigugu Turiani mkoani Morogoro tarehe 16.6.2016.
New Picture (13)Wapili kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba Nkinga akikabidhi msaada wa vitabu vilivyotolewa na asasi ya MVIWATA wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyoandaliwa na mkoa wa Morogoro katika shule ya Msingi Kigugu, wilayani Mvomero. Kushoto ni Mkuu wa wilya ya Mvomero Mhe. Betty Mkwasa akifuatiwa na viongozi wa mradi wa MVIWATA na kijiji cha Kigugu (16.6.2016).
New Picture (14)Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bibi Sihaba, wa pili kulia ni Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mhe. Betty Mkwasa, akifuatiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Watoto Bibi Magareth Musai (kulia), na kushoto ni mwenyekiti wa asasi ya MVIWATA Bw. Mgweno wakiwa wamesimama mkabala na jiwe la msingi la maktaba ya Kata ya Kigugu lililozinduliwa wakati wa kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika shule ya Msingi Kigugu Turiani, wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro tarehe 16.6.2016.
New Picture (15)Watoto wa Shule ya Msingi Kigugu wilaya ya Movomero, mkoani Morogoro wakiingia uwanjani kwa maandamano wakati wa kilelele cha Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyohudhuriwa na wakazi wa mkoa wa Morogoro katika kijiji cha Kigugu Turiani, mkoani Morogoro, siku ya Tarehe 16.6.2016.
New Picture (16)Mwenyekiti wa Baraza la Watoto mkoa wa Morogoro mtoto Aprinia M. Joseph, mwanafunzi wa (kidato cha IV) Shule ya Sekondari Mgulasi, akisoma risala ya watoto wa mkoa wa Morogoro kwa Mgeni rasmi Katibu Mkuu, wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bibi Sihaba Kinga (hayupo pichani) wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika mkoani Morogoro yaliyofanyika katika kijiji cha Kigugu,wilaya ya  Mvomero, tarehe Juni 16, 2016.

No comments:

Post a Comment