Friday, April 15, 2016

JUMA LA AFYA KATIKA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO KIMARA LAHITIMISHWA KWA BONANZA

Wiki iliyoanza jana  ilikuwa  ni ya mbaraka kwa washiriki wa Kimara Sda kwa semina za afya zilianza siku ya jumapili huku mada mbambali zikiwasilishwa na madakitari,ya kwanza ikihusisha umuhimu wa kujua ni magonjwa yatokanayo na lishe duni,ambapo mtoa mada Dr.Sabai alisisitiza lishe ni jambo muhimu sana kwa afya binadamu na semina hizi ziliendelea hadi jumamosi siku ya Sabato na siku hii watu waligawanyika katika makundi kulingana na rika lao ili iwe vyepesi kwa watoa mada waweze kujua ni nini rika husika linataka na hivyo kwa kupitia majibu ya  maswali mbalimbali toka kwa rika husika.
Jumapili baada ya semina kuisha kukawa na bonanza kubwa lilofanyika katika viwanza vya Shule ya Msingi Mavurunza Kimara Dar Es Salaam,bonanza hili lilihusisha michezo kama vile,kukimbia mbio za mita 100,mbio za kupokezana vijiti na kukimbiza kuku.
Zikianza mbio kwa namna hii hapo inahesabiwa moja,mbili,tatu jiandae ...kimbia
Inahitaji nguvu,jitahada na ubunifu na kwa mbio hizi za wanaume wa zaidi ya miaka 30 wakikimbia mbio moja kati ya michezo iliyoleta furaha na hamasa siku ya jana. 
Watoto nao hawakupenda kuachwa mbali,wako makini wasipitwe na mbio hizi zenye umbali wa mita 100 katika viwanja vya Mavurunza.
Wakina mama ni jeshi kubwa..hapa ni maandalizi ya mbio yakianza na wakisubiri mwamuzi wa mchezo ambaye ni mchungaji wa mtaa wa Kimara Rahisi Mande atoe ruksa na kufungilia mbio hizo.
Hili ni kundi la kwanza kwa mchezo wa kupokezana vijiti na hapa wakienda mbio kuwapa wenzao kundi namba mbili wakiwa mbele kabisa na katika mchezo huo Mzee Joshua Manyama ndiye aliibuka mshindi.
Mzee Manyama akiitimisha mbio hizi akiwa mbele kabisa kuwashinda wenzake na kushika nafasi ya kwanza kwa mchezo kwa kukimbia na kijiti hapo jana.
Mzee Ronard Manongi akikikimbia na kijiti katika uwanja wa Mavurunza ambapo Mzee Joshua Manyama ndiye alishinda mchezo huo.
Kushoto ni mshindi wa mbio za kukimbia na kijiti,Joshua Manyama anayefuata ni mchungaji wa mwamuzi wa michezo yote ya jana Rahisi Mande akimwelekeza mchukua taarifa za washindi na hapa wakiandika jina na Joshua Manyam.
Mama Manyama mke wa Joshua Manyama kushoto akikimbia kumkaribia kuku ambaye alifunguliwa ili wamkimbize wakina mama katika mchezo wa kukimbiza kuku lakini baadae ndiye alikuwa mshindi na kulia ni Mama Naetwe Manongi nae akikimbia kwa bidii katika mchezo huu.
Hapa ni Mama Mchungaji(kushoto) mwenye jezi ya blu anayefuata ni Diana Manyama,Asnati Ngakonda na mwisho ni Naetwe Manongi wakikimbiza kuku katika shindano la kukimbiza kuku lililofanyika jana.
Kulia ni Diana Manyama akifurahi mara baada ya kushinda katika shindano ya kuku hapo jana kushoto ni Asnati Ngakonda akimpongeza na kulia ni mtoto akishuhudia.


Furaha na bashasha zilitawala mara baada ya ushindi na Mama Diana Manyama akielekea kuhojiwa na mtangazji juu ya ushindi wake.
Kwa vijana huyu ndiye mbabe kupita wote kwa siku ya jana,kwani kijana John (kulia) alijipatia zawadi nono ya kuku aliyoshinda mara baada ya kuwashinda wenzake kwenye mchezo wa kukimbiza kuku hapo jana viwanja vya Mavurunza hapa akihojiwa juu ya ushindi wake na mtangazaji toka morning star redio Jackson Sekiete(kushoto).
Kulia ni Dr.Mathias Abuya(kulia) akiwa na kuku ambaye alimpata mara baada ya kushinda katika shindano la kukimbiza kuku na Dr.Abuya ndiye alikuwa mtoaji mada kwa juma lililopita la afya ambalo siku ya jana lilikamilishwa na bonanza la michezo mbalimbali ikiwemo kukimbiza kuku,kukimbia na kijiti na mbio za mita 100 na hapa akiwa na Jackson Sekiete mtangazaji toka Morning star redio akieleza juma la afya lilivyokuwa na mwito wa washiriki wa kanisa katika maswala ya afya akigusia huduma za vipimo vya bure kwa uchunguzi kwa magonjwa na kina mama kama vile saratani ya matiti na kizazi.
Vuta nikuvute,hapa anatafutwa mashindi katika mchezo wa kuvuta kamba,na timu upande wa kulia walishinda.

No comments:

Post a Comment