Monday, July 11, 2016

Simu milioni 10 za Android zaathiriwa na kirusi



Image captionKirusi kinachoathiri simu za Android
Hadi simu milioni 10 aina ya Android zimeambukizwa virusi vinavyotoa Clicks bandia kwa ajili ya matangazo kulingana na watafiti.
Programu hiyo pia inaweka apps na kumchunguza mwenye akaunti.
Kirusi hicho kinawapatia takriban dola 300,000 kila mwezi waliokianzisha.
Simu nyingi ambazo zimeathiriwa na kirusi hicho zipo nchini China
Ongezeko la simu zilizoathiriwa na kirusi hicho lilibainika na kampuni ya usalama wa mitandao Checkpoint na Lookout.
Kirusi hicho kinatoka familia ya Shedun by Lookout but Hummingbad by Checkpoint.
Image captionSmartphone
Katika blogu,Checkpoint imesema kuwa imefanikiwa kubaini kithibiti cha simu zilizoathiriwa ambacho kinaonyesha kuwa Hummingbad imeathiri simu milioni 10.
China ,India,Ufilipino na Indonesia zinaongoza katika mataifa yenye simu zilizoathirika.

No comments:

Post a Comment