Friday, June 10, 2016

Hakuna Record Label Ninayoweza Kukubali Inisainishe, Watanipa nini Ambacho Sijafanya! – Diamond Platnumz

Diamond Platnumz hana mpango wa kuwa chini na record label yoyote duniani. Infact hitmaker huyo amedai kuwa makampuni kibao yamewahi kummendea yakitaka awe chini yake lakini akayapiga kibuti.

“Mimi nimeshaapprochiwa na makampuni mengi sana kutaka kunisaini, mengi sana, mengi hata wanayoyasikia, mengine wanayasikia,” Diamond ameiambia 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM.

“Lakini nafikiria kwamba unapotaka kunisaini mimi unataka kunifanyia nini? Una kitu gani cha kunioffer cha kuona mimi unisaini? Video? Mimi naweza kufanya video zangu hadi za wasanii wangu. Collabo? Collabo mimi naombwa napigiwa simu, msanii wa Marekani wa Tanzania, yeyote nikitaka kufanya chochote naweza kufanya naye,” ameongeza.

“At the end of the day is all about money, nina capital, nina network, ndio maana nikasema kwa nilipofikia sio nibaki mimi tu, niwe na record label yangu. So sifikirii kusainishwa, nafikiria kusaini watu ili kuweza kusaidiana wenyewe kwa wenyewe.”

“Kwa mfano unataka kunisaini, unataka kunifanyia nini? Nikaperform mbinguni? Tuzo zote ambazo mwaafrika anatakani kuziwin.. sijawahi kupata BET na Grammy tu, nataka nipige na Grammy nioneshe kabisa napiga na Grammy. Ukiniambia nasainiwa it doesn’t make sense. Naamini management yangu ni kubwa kuliko mtu yeyote akinisaini, akisema anifanyie promotion hatoweza kufanya promotion ninayoifanya mimi,” amesisitiza.

Diamond aliyeanzisha record label yake, WCB tayari amewasaini Harmonize na Raymond huku kukiwa na uwezekano kuwa amemshamsaini Rich Mavoko.

No comments:

Post a Comment