Friday, June 10, 2016

RAIS MAGUIFULI MGENI RASMI SIKU YA KIMATAIFA YA ALBINO...........

RAIS MAGUIFULI MGENI RASMI SIKU YA KIMATAIFA YA ALBINO

al1Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wenye Alibinism Tanzania (TAS) Nemes Temba akizungumza na waandishi wa Habari (hawapopichani) leo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujulisha umma siku ya maadhimisho ya Albino duniani.Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa TAS Dar es Salaam, Gabriel Aluga, Katibu Mkuu wa TAS, Musa Katimba na Mratibu kutoka asasi ya kiraia ya BADEF.
al2Mwenyekiti wa Mfuko wa Good Hope Star na mjumbe wa kamati ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya Albino duniani Al Shamaymaa Kwegyir akifafanua jambo wakati wa mkutano wa waandishi wa Habari (hawapopichani) leo jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujulisha umma siku ya maadhimisho ya Albino duniani.Kutoka kuliani Mwenyektiwa TAS Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa TAS, Musa Katimba (kushoto) na Mwenyekiti wa  TAS Taifa Nemes Temba.
al3Wandishi wa habari wakichukua matukio wakati wa mkunano baina ya TAS na waandishi wahabari katika ukumbi wa  Idara ya Habari – MAELEZO leo jijini Dar es Salaam.
NA: Frank Shija,MAELEZO.
…………………………………………………………………………………………………………..
Na:BR,MAELEZO
Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa  kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya kuongeza uelewa kuhusu ualbino yatakayofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa chama cha Watu Wenye Ualbino Nchini  (Tanzania Albinism Society) Nemes Temba ameeleza kuwa kupitia maadhimisho hayo jamii itapata fursa ya kupewa elimu muhimu kuhusu ualbino ili kuondoka na dhana potofu hususani ushirikina.
“Maadhimisho haya ambayo yataanza Juni 11 hadi Juni 13, 2016 yatasindikizwa na mambo mbalimbali ikiwemo  huduma za afya hususani uchunguzi na matibabu ya saratani ya ngozi pamoja na nasaha za viongozi na mabalozi, utambulisho wa Miss Albino Tanzania na uzinduzi wa kamusi ya ulemavu,” alisema Temba.
Temba aliendelea kuainisha kwamba  siku hiyo itawapa fursa watoto wenye ualbino waishio kwenye vituo mbalimbali nchini kutembelea mji wa Bagamoyo kujionea mambo mbalimbali chini ya ufadhili wa shirika la UNICEF.
Aidha Mwenyekiti huyo amemshukuru Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuwapa vipaumbele watu wenye ulemavu akiwemo Dkt. Abdallah Possi ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge, Sera, Ajira, Kazi na Watu Wenye Ulemavu hii inadhihirisha kuwa ulemavu si hoja bali utendaji kazi ndio kitu umuhimu.

No comments:

Post a Comment