Monday, February 15, 2016

Kanye West aomba pesa kutoka kwa Zuckerberg

Kanye West aomba pesa kutoka kwa Zuckerberg


Kanye WestImage copyrightReuters
Image captionKanye West alisema majuzi kwamba anadaiwa $53m
Mwanamuziki Kanye West amemuomba hadharani mwaanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg ampe usaidizi wa kifedha.
West anataka Zuckerberg awekeze $1bn (£700m) katika miradi yake akisema yeye binafsi hana “rasilimali za kutosha” kuunda kile ambacho “anaweza”.
Ametoa ombi hilo siku chache tu baada ya kutangaza kwamba ana deni la $53m (£36m) alipokuwa akitoa albamu yake mpya.
West alijitetea kupitia msururu wa jumbe kwenye Twitter.
Waandishi wa BBC Newsbeat wamewasiliana na maafisa wa Facebook ambao wamesema: “Hatuna lolote la kusema kwa sasa.”
Jambo la kushangaza ni kwamba Kanye West amemuomba Zuckerberg usaidizi kupitia Twitter ambao ni mtandao unaoshindana na Facebook.

No comments:

Post a Comment