Thursday, July 16, 2015

Ulimis? maneno ya Lowassa, Membe, Makamba na Ngeleja baada ya Top 5 ya CCM kutangazwa

Ulimis? maneno ya Lowassa, Membe, Makamba na Ngeleja baada ya Top 5 ya CCM kutangazwa

By Roryamaendeleo.
Lowassahttp://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/07/Lowassa.jpg



Jana July 15 2015 mmoja wa Wanasiasa wakongwe Tanzania mzee Kingunge Ngombale Mwiru aliongea na waandishi wa habari na kusema hakuridhishwa na kitendo cha CCM kutoliingiza jina la Edward Lowassa kwenye mchujo wa kwanza wa Top 5 wa waliokua wanautaka Urais kupitia ticket ya CCM.
Mzee Kingunge alisema >>> ‘Kamati Kuu inapelekewa orodha ya watu watano wapitishwe, hawa Wagombea wote 38 waliorudisha fomu hawakuwaona, hawakupita mbele yao, hawakuwauliza maswali na hata kwenye Kamati ya Maadili naamini hawakuitwa.. Kuna watu wachache wamekaa wakatengeneza orodha yao’
Pamoja na hayo, hii hapa chini ni video ikiwaonyesha Edward Lowassa, January Makamba, William Ngeleja na Bernard Membe wakizungumza baada ya Top 5 kutangazwa na list ikawataja January Makamba, Bernard Membe, Balozi Amina Salum, Asharose Migiro na John Magufuli.

No comments:

Post a Comment